nEWS nAIROBI kENYA: Odinga avaa kofia ya Kenyatta, atangaza kesho siku ya mapumziko nchi nzima...#share

ALIYEKUWA mngombea wa kiti cha Urais nchini Kenya kwa tiketi ya Muungano wa Vyma vya Upinzani (NASA) amatangaza kesho kuwa siku ya mapumziko nchi nzima.


Ametoa kauli hiyo mapema leo akizungumza na wafuasi wa NASA wakati akitoa salamu za lambalambi kwa familia iliyofiwa na mtoto wao Moraa Nyaranga (10).

NASA wamedai kuwa mtoto huyo ameuawa kwa kupigwa risasi jana na askari polisi.

Tangu kutangazwa kwa Uhuru Kenyatta kuwa mshindi wa Urais kwa awamu ya pili nchini Kenya, kumekuwa na maandamano ya wafuasi wa NASA wakidai kuibiwa kura hali ambayo imepelekewa kuwa na makabiliano baina ya polisi na waandamanaji.

Aidha kauli hiyo imekuja kukiwa na taarifa kwenye baadhi ya mtandao nchini Kenya zinadai hadi leo zaidi ya wananchi 20 wamepoteza maisha katika maeneo mbalimbali nchini humo kutokana na kuzuka kwa ghasia za kupinga matokeo ya uchaguzi huo.

Alhamisi iliyopita, NASA ilidai Odinga ndiye aliyeshinda uchaguzi huo na kuitaka IEBC kumtangaza kuwa mshindi.

Katika uchaguzi huo Rais Kenyatta alipata kura 8, 203, 290 ambazo ni asilimia 54.27 huku Odinga akapata kura milioni 6,762,224 sawa na asilimia 44.74.
Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search