tREANDING nEWS: Kofi Annan ampa mbinu Odinga kuingia IKULU Kenya...#share


KATIBU Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa (UN) Kofi Annan, ametoa wito kwa muungano wa vyama vilivyoshindwa kwenye Uchaguzi Mkuu nchini humo kutumia mifumo ya kisheria kutafuta haki.


Annan alikuwa mpatanishi mkuu wa mzozo wa kisiasa nchini Kenya miaka kumi iliyopita, baada ya ghasia kuzuka kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2007 uliokumbwa na utata ambapo Rais mstaafu Mwai Kibaki alitangazwa mshindi wakati huo huku Raila Odinga na chama chake cha ODM na muungano wa vyama vya NASA wakapinga matokeo hayo.

Katika taarifa yake Annan amempongeza Rais Uhuru Kenyatta kwa ushindi huku akamsifu kiongozi wa NASA, vinavyolalamikia hujuma kwenye uchaguzi huo, kwa kuendesha kampeni yake kwa njia ya amani.

"Namshukuru kiongozi wa upinzani Odinga kwa kampeni ya uchaguzi ya amani aliyoiendesha. Amekuwa mtetezi jasiri wa demokrasia," alisema Annan kupitia taarifa yake.

Ameongeza: "Hivyo, namhimiza sasa afuatilie malalamiko yake kupitia mifumo ya kisheria iliyowekwa na aweke maslahi ya taifa mbele, kama alivyofanya awali kwa uzalendo na mara nyingi,”

Annan amesema upinzani umekuwa ukidai mitambo ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), ilidukuliwa na matokeo kuchakachuliwa ili kumpa ushindi Rais Kenyatta.

Wakati Annan akitoa rai hiyo kwa NASA taarifa za baadhi ya mtandao nchini Kenya zinadai hadi leo zaidi ya wananchi 20 wamepoteza maisha katika maeneo mbalimbali nchini humo kutokana na kuzuka kwa ghasia za kupinga matokeo ya uchaguzi huo wa Agosti nane.

Alhamisi iliyopita, NASA ilidai Odinga ndiye aliyeshinda uchaguzi huo na kuitaka IEBC kumtangaza kuwa mshindi.
Katika uchaguzi huo Rais Kenyatta alipata kura 8, 203, 290 ambazo ni asilimia 54.27 huku Odinga akapata kura milioni 6,762,224 sawa na asilimia 44.74.


Mawakala wakuu wa NASA waliondoka ghafla katika kikao cha tume hiyo cha kuafikiana kuhusu matokeo hayo kabla ya kutangazwa kwa Kenyatta kuwa mshindi wa uchaguzi huo.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search