nEWS: NEC yafanya uteuzi Madiwani wanawake viti maalum 12....Jua Majia, Halmashauri na Vyama vyao....#share

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIATUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UTEUZI WA MADIWANI WANAWAKE WA VITI MAALUM.


Kwa Mujibu wa Kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika kikao chake cha kawaida kilichofanyika leo tarehe 21 Agosti, 2017 na baada ya kushauriana na Vyama vya Siasa imewateua Madiwani Wanawake wa Viti Maalum kumi na wawili (12) kujaza nafasi wazi za Madiwani katika Halmashauri mbalimbali Tanzania Bara.

Madiwani Wanawake wa Viti Maalumu walioteuliwa ni kama ifuatavyo:
NA.
JINA
CHAMA
HALMASHAURI
1.  1
Ndugu Saida Idrisa Kiliula
CUF
Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa
Ndugu Sophia Charokiwa Msangi
CCM
Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
Ndugu Shahara Selemani Nduvaruva
CCM
Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali
Ndugu Neema K. Nyangalilo
CCM
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala
Ndugu Farida Zaharani Mohamed
CCM
Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero
Ndugu Lucia Silanda Kadimu
CCM
Halmashauri ya Wilaya ya Tabora (Uyui)
Ndugu Amina Ramshi Mbaira
CCM
Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu
Ndugu Janeth John Kaaya
CHADEMA
Halmashauri ya Wilaya ya Meru
Ndugu Sara Abdallah Katanga
CHADEMA
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala
Ndugu Ikunda Massawe
CHADEMA
Halmashauri ya Wilaya ya Hai
Ndugu Tumaini Wilson Masaki
CHADEMA
Halmashauri ya Wilaya ya Siha
Ndugu Elizaberth Andrea Bayyo
CHADEMA
Halmashauri ya Mji wa Mbulu

Uteuzi huu umefanyika baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa ambaye kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 alitaarifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi uwepo wa nafasi hizo wazi.
 Imetolewa leo tarehe 21 Agosti, 2017

Kailima, R. K
MKURUGENZI WA UCHAGUZI


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search