sPOTRS : Jua wachezaji 8 wakuchungwa kuelekea mtanange wa Simba na Yanga ngao ya jamii kesho kutwa...#share


Wakati tukielekea kutizama mpambano wa ufunguzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara (Ngao ya Jamii) katika ya Simba na Yanga, wafuatao ni wachezaji wa kuchungwa na pande zote.
Simba  na Yanga zitashuka dimbani siku ya Jumatano, Agosti 23 uwanja wa Taifa Dar es salaam kwa ajili ya mchezo wa kuwania Ngao ya Jamii.


Ukiachana na historia ya pambano hilo, pia ukubwa wa mtanange huo unatokana na nyota wapya waliopo kwenye klabu zote mbili.

Timu zote mbili zinatarajiwa kuwakosa nyota wake muhimu wa kikosi cha kwanza kutokana na majeraha wanayouguza, Kakolanya, Mwashiuya na Chirwa kwa upande wa Yanga wanatarajiwa kukosekana huku Bocco, Kapombe, Mohammed Hussein kwa upande wa Simba wakiwa na asilimia kubwa ya kuukosa mchezo huo.

Hawa ndiyo wachezaji 8 wa kuchungwa kuelekea mchezo wa Yanga na Simba.

Amissi Tambwe - Yanga
Amekuwa na rekodi nzuri ya kuifunga Simba tangu ajiunge na Yanga misimu 3 nyuma, Mrundi huyo anaitaji ulinzi mkubwa kumzuia hasa kwa mipira ya hewani, kama kona na krosi.

Shiza Kichuya - Simba
Ni mwiba kwa upande wa Yanga siku ya Jumatano, mechi mbili za mwisho winga huyo aliibuka shujaa, safu ya ulinzi ya Yanga inaitaji umakini mkubwa na kutoruhusu kufanya faulo maeneo ya karibu kwani, Kichuya ni mpigaji wa mipra ya adhabu.

Donald Ngoma - Yanga
Ni mshambuliaji mwenye kasi, nguvu na jicho la goli, pia ni mzuri kwenye mashambulizi ya kushutukiza, ana tazamiwa kuwa mwiba kwa Simba kama asipowekewa ulinzi dhabiti wa kumzuia.

Emmanuel Okwi - Simba
Okwi ni mchezaji hatari sana kasi yake, krosi murua na umakini wa kufunga amekuwa akiwapa tabu mabeki wengi hivyo safu ya ulinzi ya Yanga inaitaji umakini wa kumdhibiti.

Thabani Kamusoko -- Yanga
Ndiye kiunganishi wa timu ya Yanga, kuanzia safu ya ulinzi hadi ushambuliaji, hatakiwi kuwa huru kufanya anachotaka kwani ndiye mwenye mipango yote ya klabu ya Yanga.

Haruna Niyonzima - Simba
Amejiunga na Simba akitokea Yanga, Harruna anatazamiwa kuwa mwiba kwa upande wa Yanga kama asipowekewa ulinzi mkali, ni mchezaji mbunifu mwenye uwezo wa kufunga, na kutengeneza nafasi kwa washambuliaji.

Ibrahim Ajibu - Yanga
Siyo mshambuliaji wa kupewa nafasi muda wote, Ajibu ni mmoja wa nyota wachache kwenye Ligi Kuu wenye uwezo mkubwa wa kumiliki mpira kutokana na ubunifu wake mkubwa.

Mzamiru Yassin - Simba
Ni mchezaji ambaye atamkwi sana, ila ni mmoja wa nyota wa kuangaliwa sana kwani mechi nyingi ngumu kwa upande wa Simba amekuwa ndiye msaada mkubwa sana.

Na Jerry Mlosa/Goal Tanzania



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search