nEWS: Rais wa TLS Tundu Lissu awashambulia vikali Mawakili waliopuuza Mgomo wa kutokwenda Mahakamani leo na kesho...Atoa kauli nzito dhidi yao...#share
RAIS wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) Tundu Lissu,
amesema mawakili waliokwenda katika Mahakama na Mabaraza ya aina zote
kutekeleza majukumu yao ya uwakili ni ishara kuwa wanaunga mkono utawala wa
mabomu nchini.
Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam akizungumza na
waandishi wa habari baada ya Tamko la Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu
(LHRC) la kukemea na kulaana shambulio dhidi ya Ofisi za IMMMA Advocates
lililotokea hivi karibuni.
Aidha amesema kuwa mawakili hao watakuwa hawaungi mkono
jitihada za kuhakikisha kunakuwepo usalama wa mawakili katika kutekeleza
majukumu yao ya uwakili.
“watakuwa wanasema kwamba ni sawasawa ofisi za mawakili
kupigwa mabom, watakuwa wanasema ni sawasawa kwa mawakili kushambuliwa, watakuwa
wanasema kwamba ni sawasawa kwa mawakili kupotea,” amesema Lissu.
Amebainisha tamko la kususia kuhudhuria mahakamani na kwenye
mabaraza ya aina zote kwa siku mbili leo na kesho walilitoa kama viongozi waliopewa dhamana ya uongozi na
mawakili nchini hivyo walidhani tukio hilo la shambulio ni kubwa la kuwafanya
wapeleke ujumbe kwa jinsi hiyo.
“Kama kuna wakili anadhani kwamba tumekosea anahaki ya
kuamini hivyo,” amesema Lissu.
Ameongeza kwa kusema kuwa lengo la mgomo ni huo ni kutoa
ishara ya kutoukubali utawala wa mabomu nchini huku akiwataka mawakili wanaofikiri
kilichotokea kuwa ni kitu cha kawaida waendelee
kudhani hivyo.
Aidha amesema baada ya mgomo huo wataendelea kufuatilia suala
hilo ikiwa ni pamoja na kufanya mkutano na vyombo vya usalama ili kuwaeleza
hofu waliyonayo kama mawakili.
Na Abraham Ntambara
No comments:
Post a Comment