POLISI: Jeshi la Polisi leo limetaja sababu Tundu Lissu kupimwa mkojo kwa Mkemia Mkuu wa Serikali akiwa na kosa la uchochezi...#share
KAMADA wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna
Msaidizi wa Jeshi la Polisi Lazaro
Mambosasa ametaja sababu ya kumpeleka mtuhumiwa wa kesi ya uchochezi kupimwa mkojo kwenye Ofisi ya Mkemia
Mkuu wa Serikali.
Hivi karibuni Mwanasheria Mkuu wa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Rais wa Chama cha Wanasheria wa
Tanganyika (TLS) Tundu Lissu, Jeshi la Polisi lilimpeleka kumpima mkojo kwa
Mkemia Mkuu wa Serikali huku ikifahamika kuwa anashutumiwa kwa kosa la
uchochezi.
Akizungumza leo wakati akijitambulisha kwa waandishi wa
habari na wananchi wa jijini humo kama Kamanda Mpya wa Mkoa huo, amesema kuwa
lengo la kumpima mkojo ni kutaka kujua kama mtu huo anafanya hayo akiwa na
akili zake timamu au la.
Aidha amesema kwamba matumizi ya vileo na dawa za kulevya vinaweza
kumfanya mtu kuropoka hovyo kutokana na kwamba matumizi ya vitu hivyo huchangia
mtu kupoteza au kupungua busara zake.
“Vileo vya pombe na dawa za kulevya watumiaji wake hawako salama busara zao hupungua,”
amesema Mambosasa.
Amesema kutokana na sababu hiyo mtuhumiwa wa jinsi hiyo
hupelekwa kwa Mkemia kubaini iwapo anatumia moja ya vitu hivyo ili kujua kama
ndiyo chanzo cha yeye kuongea lolote anapojisikia pasipo kuzingatia utaratibu.
Na Abraham Ntambara
No comments:
Post a Comment