nEWS: Shambulio dhidi ya Ofisi za Mawakili ya IMMMA Advocates latua kwa Dk. Bisimba na LHRC yake..Atoa Tamko kali dhidi ya tukio hilo..Pia aunga Mkono Mgomo wa Mawakili ulioanza leo na kesho...#share

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na wadau wengine wa haki za binadamu kimekemea na kulaana vikali shambulio dhidi ya Ofisi ya Mawakili wa IMMMA  Advocates  huku kikitoa mapendekezo saba kwa serikali ili kuimarisha utawala bora nchini.


Aidha kimemshauri Rais John Magufuli kumteua Jaji Mkuu kwa mujibu wa Katiba ili kuimarisha mhimili wa mahakama na utawala wa sheria.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jinni Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC  Dr. Hellen Bisimba amesema shambulio hilo linahatarisha utetezi wa haki ya uwakilishi na uwezo wa wanasheria kutekeleza majukumu yao bila vitisho.

“Kanuni ya 16 ya Kanuni za Msingi za Umoja wa Mataifa juu ya Wajibu wa Wanasheria za 1990 (UN Basic Principles on the Role of Lawyers 1990) inasema kwamba Serikali zitahakikisha kwamba wanasheria wanatekeleza majukumu yao bila vitisho, vikwazo au kuingiliwa kinyume na sheria,”

“Pia, Kanuni hiyo inakataza wanasheria kutishiwa kushtakiwa au kuwekewa vikwazo vya kiuchumi au kiutawala pale wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kikazi,” alisema Bisimba.

Kufuatia tukio hilo Bisimba amesema Jumuiya ya watetezi wa haki za binadamu imepatwa na wasiwasi mkubwa kuhusu hali ya usalama na ulinzi wa haki za binadamu nchini, ikiwemo uminywaji wa uhuru wa wanasheria na haki ya uwakilishi.

Kutokana na hali hiyo LHRC imetoa mapendekezo saba kwa serikali kwa ajili ya kuimarisha hali ya ulinzi na usalama wa haki za binadamu nchini. Bisimba alitaja mapendekezo hayo kuwa ni, Serikali, kupitia Jeshi la Polisi, kuhakikisha watu ambao wamehusika na shambulio la Ofisi ya Mawakili ya IMMMA Advocates wanakamatwa nakuchukuliwa hatua kali za kisheria haraka iwezekanavyo.

Amesema nyingine ni Tasnia ya Sheria iachwe huru katika kufanya kazi zake na kupatiwa ulinzi kwa mujibu wa sheria na wanasheria waachwe watekeleze majukumu yao bila kuingiliwa wala kutishiwa.

Mahakama kama mhimili muhimu katika usimamizi wa haki, ina wajibu wa kuhakikisha kwamba maofisa wote wanafanya kazi chini ya mhimili huo wanakuwa salama na wanalindwa kwa mujibu wa sheria katika kutekeleza majukumu yao.

Kumshauri Rais John Magufuli kumteua Jaji Mkuu kwa mujibu wa Katiba, ili kuimarisha mhimili wa Mahakam na utawala wa sheria.
Mengine ni Viongozi wa serikali na vyombo vyake wenye dhamana ya kulinda usalama wa watu nchini na haki za binadamu kwa ujumla wawajibike au kuwajibishwa mara moja pale ambapo wameshindwa kusimamia ipasavyo majukumu yao kwani wanasikitika hadi jana kutosikia kauli rasmi ya serikali kulaani kitendo hicho.

Aidha amewataka wananchi kuwa mstari wa mbele kuripoti matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu na uhalifu, ikiwemo mauaji mbalimbali yenye utata kwa vyombo vya dola na vituo vya kutetea haki za binadamu bila woga.

Ametoa wito kwa wananchi wote wenye mapenzi mema wakiwemo mawakili wakemee vitendo kama hivyo kwani vinaathari kwa kila mwananchi.



Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search