sPORTS nEWS: Haji Manara amnyooshea Mikono Kamsoko wa Yanga....Adai si mchezaji watanzania....#share

OFISA Habari wa Klabu ya Simba Haji Manara amedai kuwa wa Kimataifa wa Klaby ya Yanda Mzimbabwe Thabani Michael Kamusoko hana hadhi ya kucheza mpira katika vilabu vya Tanzania.


Manara amesema hayo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram kwamba anatakiwa kucheza ulaya kutokana na mchezaji huyo kuwa na jitihada pamoja na umahiri mzuri wa kusakata kabumbu uwanjani.

"Huwa sifichi mahaba yangu kwa mchezaji anayenivutia uwanjani hata kama anachezea klabu nisiyoishabikia. Scara Kamusoko hapewi heshima anayostahili nchi hii. 'Level' yake ni kucheza Ulaya", ameandika Manara.

Kamusoko ni mmoja miongoni mwa wachezaji wa klabu ya Mtaa wa Twiga na Jangwani Yanga ambao wamekuwa wakionyesha kiwango kizuri na kuisaidia klabu katika mashindano mbalimbali.


Aidha mchezaji huyo ameweza kuonyesha kiwango kizuri  jana katika mechi ya ufunguzi wa michuano ya Ligi Kuuu Tanzania Bara dhidi ya Lipuli FC ambapo klabu hizo zilitoka  sare ya mabao 1-1 katika mchezo ulipigwa katika dimba la Taifa Jijini Dar es Salaam.



Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search