nEWS: TABOA wamjaribu JPM.....Wagomea Mashine za Kielekroniki kukatia tiketi za Mabasi.....#share


MKUTANO Mkuu wa Chama cha wamiliki wa mabasi (TABOA) umeazimia kwa kauli moja kupinga mpango wa matumizi ya mashine za kieletroniki katika ukatishaji wa tiketi kwa abiria wanaotumia mabasi hayo hadi pale watakapomaliza tofauti zao na serikali.


Kwa mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa TABOA, Abdalah Mohamed tofauti hizo ni zile zinatokana na changamoto ya matumizi ya mashine za kieletroniki ambapo ni lazima eneo husika kuwa na huduma za Internet ilihali huduma hiyo haipatikani vizuri maeneo yote nchini hivyo ipo hatari ya watu kushindwa kupata tiketi iwapo maeneo waliyopo hayana huduma hiyo.

Kutokana na hali hiyo wajumbe wa mkutano huo mkuu wa TABOA wakaingia katika majadiliano makali huku baadhi wakitaka mkutano mkuu mwingine wa dharura uitwe huku mawaziri wenye dhamana ya ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano na yule mwenye dhamana ya fedha na mipango na wasaidizi wao wawepo ili kulijadili suala hilo na kulipatia ufumbuzi.

Hata hivyo mkutano huo ukaunga mkono hoja ya Naibu Katibu mkuu wa TABOA, Issa Nkya ya kutolewa wiki moja kwa kamati maalum ya TABOA ambayo ilikuwa imeundwa kufuatilia suala hilo wamalizane na mamlaka ya mapato Tanzania -TRA kupitia kamishina mkuu wa kodi na ikishindikanika wachukue hatua nyingine.

 Na Muungwana.blog

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search