sPORTS nEWS: Chiji wa Simba na Yanga atimukia Coastal Union...#share
TIMU ya soka ya Coasta Union ya
Jijini Tanga, itaanza mazoezi kesho (Jumanne) kwenye uwanja wa Mkwakwani
kujiwinda na Ligi Daraja la Kwanza (FDL), inayotarajiwa kuanza mwezi ujao huku
ikitangaza nyota wake wapya iliyowasajili msimu huu.
Aurora amewataja baadhi ya
wachezaji wapya kuwa ni pamoja na mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ‘Taifa
Stars’, Simba na Yanga Athumani Idd ‘Chuji’, Hussein Sharrif ‘Cassilas’,
Salvatory Ntebe kutoka Ndanda FC, Ramadhani Hassain kutoka Mbeya City, Maulid
Rajab ‘Mau’ African Sports, Hilal Juma Mtibwa, Ramadhani Mussa Pamba, Ibrahim
Ndanda, Baraka Jafar na Omary Salum kutoka African Lyion.
Aurora ametaja wachezaji
wengine ni pamoja na mfungaji bora wa Ndondo Cup iliyomalizika hivi karibuni
Jijini Dar es salaam Rashid Roshi, Exavery Emanuel, Rahim Aziz Afrikan Lyon, Sagaf
Kabaki, Bakari Mtwiku, Bakari Nondo, Said Jeilani na Abubakari Kinanda ‘Mapara’
kutoka malindi ya Zanzibar.
Mwenyekiti huyo amesema usajili
waliofanya ulizingatia mahitaji yaliyopo pamoja na tathimini waliyofanya baada
ya kushuka daraja na kisha mwaka jana kushindwa kurejea Ligi kuu lakini pia
umefanyika baada ya kuzika makundi yao na mpasuko.
Katibu wa klabu hiyo Nassor
Kibabedi amesema mazoezi yataanza kesho kwenye uwanja wa Mkwakwani asubuhi
kishajioni yatafanyika kwenye uwanja wa shule ya sekondari Galanos ambako
mwalimu atakuwa Joseph Lazaro




No comments:
Post a Comment