nEWS: Waziri Mkuu Kassim Majaliwa awataka wawekezaji wanaotaka kuwekeza nchini kufuata sheria, kanuni na taratibu...#share
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watu wote wenye
nia ya kutaka kuwekeza katika miradi mbalimbali nchini Tanzania kuhakikisha
wanafuata sheria, kanuni na taratibu.
Alitoa kauli hiyo jana alipokutana na kufanya
mazungumzo na Makamu wa Rais (Uendelezaji Bishara) wa Kampuni ya PIRIOU, Michel
Perrin.
Waziri Mkuu alikutana na Perrin jijini Paris nchini
Ufaransa kupitia Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa. Kampuni ya
PIRIOU inataka kuja nchini kuwekeza katika utengenezaji na ukarabati wa
meli.
Akizungumza na muwekezaji huyo Waziri Mkuu alimshukuru
kwa nia yake ya kutaka kuwekeza nchini, ambapo alimtaka afuate sheria, kanuni
na taratibu za uwekezaji nchini.
“Tanzania ni sehemu nzuri ya uwekezaji kwa sababu kuna
fursa nyingi. Pia ni nchi yenye amani na utulivu wa kisiasa pamoja na mazingira
mazuri ya uwekezaji hivyo nakukaribisha sana,”alisema.
Kwa upande wake, Perrin alisema ameamua kuja kuwekeza nchini kwa kuwa
Tanzania ni nchi salama na kwamba anauhakika wa kupata soko ndani ya nchi
pamoja na mataifa jiraji.
Alisema anaamini uwekezaji wake nchini Tanzania
utakuwa na tija, hivyo ameahidi kufanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na
Serikali na pia atahakikisha anafuata sheria zote za nchi.
Perrin alitumia fursa hiyo kumshukuru Balozi wa
Tanzania nchini Ufaransa, Balozi Samuel Shelukindo kutokana na ushirikiano
anaompa kuhusu masuala ya uwekezaji nchini.
Naye
Balozi Shelukindo alisema ataendelea kutafuta wafanyabiashara mbalimbali na
kuwashawishi waje kuwekeza katika sekta mbalimbali nchini.
Na Mwandishi Wetu
No comments:
Post a Comment