Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba aliagiza Jeshi la Magereza Kuangalia uwezekano wa kuwaajiri wafungwa wenye Ujuzi...Naye Lema atoa neno.....#share
WAZIRI wa Mambo
ya Ndani, Mwigulu Nchemba amelitaka Jeshi la Magereza kuangalia uwezekano wa
kuanza kuwaajiri wafungwa wenye ujuzi wanapomaliza kutumikia adhabu zao kwa
kuwapatia mikataba maalumu, badala ya kutumia muda mwingi kuwafundisha wafungwa
wapya.
Mwigulu amesema
Magereza wakianza utaratibu huo, utasaidia kuwa na uzalishaji zaidi wa bidhaa
pia kuendeleza tabia njema walizofundishwa wafungwa walipokuwa wakitumikia
adhabu jambo ambalo pia litawasaidia kutofanya makosa mengine kwani watakuwa
wanashughuli maalum itakayowaingizia kipato cha uhakika kila mwezi hivyo
kutoshawishika kufanya makosa ya awali yaliyowapelekea kufungwa magereza.
Aidha,
amelitaka jeshi hilo kujenga utamaduni wa kujitegemea kwa kuzalisha mali kupitia
miradi ya kilimo hatua ambayo itasaidia kupunguza utegemezi serikalini. Waziri
Mwigulu wakati alitoa rai hiyo alipokuwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi
wa nyumba tano za makazi ya askari magereza ,zilizojengwa kwa gharama ya Sh
milioni 261.
Amesema ipo
haja kwa Magereza yote nchini kuwatumia wafungwa wenye ujuzi pindi
wanapomaliza vifungo vyao na kurekebishika kwa kuwapa mikataba ya kazi na
kuepuka kila mwaka kutumia wafungwa wapya kuwapatia elimu ya ujuzi kwani pindi
wanapomaliza kutumikia vifungo, gereza linabaki halina wataalamu.
Kamishina
Jenerali wa Magereza, Dk.Juma Malewa alisema magereza nchini yanauhitaji wa
nyumba za makazi 9,800 mbali ya nyumba 4,221 zilizopo.
Amesema jeshi
hilo limeamua kujitegemea kuitikia wito wa rais John Magufuli kwa kuanza
kuwatumia wafungwa katika kutekeleza miradi mbalimbali inayotokana na kilimo na
ufugaji.
Mkuu wa Gereza
Kuu la Arusha,(RPO),Hamis Mkubasi alisema ujenzi wa mradi wa nyumba hizo
umegharimu kiasi kiasi cha Sh milioni 261,247,000 fedha zilizotokana na faida
wanayozalisha kutokana na mradi wa kilimo wa magereza mkaoni hapa.
Amesema mradi
huo ulianza kutekelezwa Machi 3,mwaka huu kwa kutumia mafundi ambao ni wafungwa
pamoja na askari magereza, hivyo kuokoa asilimia 50 ya gharama ambazo
zingetumika.
Amesema
katika katika Gereza la Arusha wana uhitaji wa nyumba 13 za askari wake
zitakazo gharimu kiasi cha shilingi milioni 675 na kutoa rai kwa mkuu wa
gereza nchini kuangalia uwezekana wa kuwapatia fedha ili wafanikishe kupunguza
changamoto ya askari kutokuwa na nyumba za makazi.
Mbunge wa
Arusha mjini, Godbles Lema amemweleza Waziri Mwigulu changamoto zilizoko katika
Gereza la Kisongo na kuitaka Serikali kuangalia umuhimu wa kuwatumia mahabusu
na wafungwa katika kufanikisha upelelezi wa matukio yanayojitokeza uraiani.
Pia aliwataka
kuweza kutumia taarifa za wananchi walioko uraiani ili kuwezesha kupata taarifa
ambazo zitamaliza changamoto mbalimbali zilizoko kwenye gereza hilo kwani nae
alituhumiwa na kukaa magereza takriban miezi minne nakufahamu zaidi halihalisi
ya magereza.
Ameshauri
Serikali kuondoa kipengere kinachozuia mtuhumiwa kukosa dhamana kutokana na
shtaka linalomkabili ili kupunguza msongamano wa mahabusu katika magereza
mbalimbali hapa nchini.
Na Mawandishi Wetu
No comments:
Post a Comment