Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba aliagiza Jeshi la Magereza Kuangalia uwezekano wa kuwaajiri wafungwa wenye Ujuzi...Naye Lema atoa neno.....#share

WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amelitaka Jeshi la Magereza kuangalia uwezekano wa kuanza kuwaajiri wafungwa wenye ujuzi wanapomaliza kutumikia adhabu zao kwa kuwapatia mikataba maalumu, badala ya kutumia muda mwingi kuwafundisha wafungwa wapya.


Mwigulu amesema Magereza wakianza utaratibu huo, utasaidia kuwa na uzalishaji zaidi wa bidhaa pia kuendeleza tabia njema  walizofundishwa wafungwa walipokuwa wakitumikia adhabu jambo ambalo pia litawasaidia kutofanya makosa mengine kwani watakuwa wanashughuli maalum itakayowaingizia kipato cha uhakika kila mwezi hivyo kutoshawishika kufanya makosa ya awali yaliyowapelekea kufungwa magereza.

Aidha, amelitaka jeshi hilo kujenga utamaduni wa kujitegemea kwa kuzalisha mali kupitia miradi ya kilimo hatua ambayo itasaidia kupunguza utegemezi serikalini. Waziri Mwigulu wakati alitoa rai hiyo alipokuwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa nyumba tano  za makazi ya askari magereza ,zilizojengwa kwa gharama ya Sh milioni 261.

Amesema ipo haja kwa Magereza yote nchini kuwatumia wafungwa wenye ujuzi  pindi wanapomaliza vifungo vyao na kurekebishika kwa kuwapa mikataba ya kazi na kuepuka kila mwaka kutumia wafungwa wapya kuwapatia elimu ya ujuzi kwani pindi wanapomaliza kutumikia vifungo, gereza linabaki halina wataalamu.

Kamishina Jenerali wa Magereza, Dk.Juma Malewa alisema magereza nchini yanauhitaji wa nyumba za makazi 9,800 mbali ya nyumba 4,221 zilizopo.

Amesema jeshi hilo limeamua kujitegemea kuitikia wito wa rais John Magufuli kwa kuanza kuwatumia wafungwa katika kutekeleza miradi mbalimbali inayotokana na kilimo na ufugaji. 

Mkuu wa Gereza Kuu la Arusha,(RPO),Hamis Mkubasi alisema ujenzi wa mradi wa nyumba hizo umegharimu kiasi kiasi cha Sh milioni 261,247,000 fedha zilizotokana na faida wanayozalisha kutokana na   mradi wa kilimo wa magereza mkaoni hapa. 

Amesema mradi huo ulianza kutekelezwa Machi 3,mwaka huu kwa kutumia mafundi ambao ni wafungwa pamoja na askari magereza, hivyo kuokoa asilimia 50 ya gharama ambazo zingetumika. 

Amesema katika katika Gereza la Arusha wana uhitaji wa nyumba 13 za askari wake zitakazo gharimu kiasi cha shilingi milioni  675 na kutoa rai kwa mkuu wa gereza nchini kuangalia uwezekana wa kuwapatia fedha ili wafanikishe kupunguza changamoto ya askari kutokuwa na nyumba za makazi.
Mbunge wa Arusha mjini, Godbles Lema amemweleza Waziri Mwigulu changamoto zilizoko katika Gereza la Kisongo na kuitaka Serikali kuangalia umuhimu wa kuwatumia mahabusu na wafungwa katika kufanikisha upelelezi wa matukio yanayojitokeza uraiani.

Pia aliwataka kuweza kutumia taarifa za wananchi walioko uraiani ili kuwezesha kupata taarifa ambazo zitamaliza changamoto mbalimbali zilizoko kwenye gereza hilo kwani nae alituhumiwa na kukaa magereza takriban miezi minne nakufahamu zaidi halihalisi ya magereza.

Ameshauri Serikali kuondoa kipengere kinachozuia mtuhumiwa kukosa dhamana kutokana na shtaka linalomkabili ili kupunguza msongamano wa mahabusu katika magereza mbalimbali hapa nchini.

Na Mawandishi Wetu



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search