sPORTS nEWS: Baada ya Manchester United kupokea kichapo toka kwa Real Madrid, Matic ampa Tano Lukaku..#share


Licha ya Klabu ya Manchester United kufungwa jana, Nemanja Matic anauhakika kuwa mchezaji mwenzake Romelu Lukaku atakuwa mtambo wa kufunga magoli katika msimu ujao.


Mashetani Wekundu jana usiku walipoteza mbele ya Klabu ya Real Madrid kwa kipigo cha goli 2-1 kwa magoli ya Casemiro na Isco kabla ya Lukaku kuirudisha mcezoni timu yake ya Manchester United baada ya kufunga goli dakika ya 62 ya mchezo.

Mshambuliaji huyo namba tisa alifunga goli la kwanza la mashindano ndani ya kikosi chake cha United United katika mchezo wenye ushindani ambapo alifunga kwa kupiga shuti baada ya shuti kali la Matic kutemwa mbele yake na Goli kipa wa Real Madirid   Keylor Navas.

Kabla ya kufunga goli hilo Lukaku alikosa nafasi ya wazi, lakini baada ya mchezo huo Matic alikuwa na Imani kwamba goli la  Mbeligiji ndiyo mwanzo wa magoli mengine.

 “Ni jambo la muhimu sana kwetu kwa mshambuliaji wetu kufunga magoli,” Matic ameiambia “Ni muhimu sana kwa kujiamini.

“Kama unavyojua alikosa nafasi nzuri,  lakini hilo linaweza kutokea, ni mpira. Lakini ninafuraha kwa kwa yeye kufunga baada ya kukosa nafasi ya kwanza na ni kwamba atafunga magoli mengi msimu huu,” amesema.

Vijana hao wa Jose Mourinho kwa sasa wanaelekeza nguvu zao kwa ajili ya maandalizi ya kuanza kwa msimu wa Ligi Kuu ya Uingeleza na Mwishoni mwa wiki hii Juma Pili watafungua Ligi kwa Mtanange dhidi ya West Ham Old Trafford. 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search