sPORTS nEWS: Barcelona wamshika pabaya Neymar wa PSG....Sasa kumburuta Mahakamani...#share



Klabu ya Barcelona imesema kuwa inatarajia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mchezaji wao wa zamani aliyetimukia klabu ya Paris Saint–German (PSG) Neymar kwa kukiuka mkataba wake.
ar

Barcelona wamebainisha kuwa wamedhamiria kumshitaki mchezaji huyo ili awalipe fidia ya paundi milioni 7.8 kwa madai kuwa alikiuka mkataba wake kwa kujiunga na PSG.
Mchezaji huyo wa kiamtaifa wa Brazili alikamilisha uhamisho wake kutoka Barca kwenda PSG mapema mwezi huu dau la paundi milioni 198 lililohitajika kuvunja mkataba wake lilipotolewa.

Barca walijaribu kufanya kila kilichowezekana kumzua mchezaji wao muhimu kuondoka, Kigogo wa La Liga Javier Tebas aliingilia kati lakini hawakuweza kumzua Neymar kuwa mchezaji ghali zaidi duniani.

Hata hivyo, uhamisho huo mkubwa zaidi wa majira ya joto umechukua sura mpya kwani Barcelona wanachunguza hasara ya euro milioni 8.5 zinazohusishwa na malipo aliyopewa mchezaji huyo kama sehemu ya bonasi ya kuhuisha mkataba wake aliposaini mkataba mpya mwaka jana.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye tovuti ya Barcelona imesema: "FC Barcelona imetoa madai dhidi ya Neymar kwa kukiuka mkataba wa RFEF (Shirikisho la Mpira wa Miguu la Hispania) na imeshaifahamisha FIFA na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Ufaransa (FFF).

"Klabu inamdai mchezaji kurejesha fedha alizolipwa kama sehemu ya bonasi kwani hajatimiza masharti ya mkataba wake. Kiasi cha euro milioni 8.5, jumlisha riba ya 10%. Klabu imeitaka PSG kufidia kiasi hicho cha fedha ikiwa mchezaji huyo hatawajibika kufanya hivyo.

"FC Barcelona imechukua hatua hii ili kulinda maslahi ya klabu baada ya Neymar kuvunja mkataba wake na klabu ndani ya miezi michache tu baada ya kusaini mkataba mpya hadi 2021."

Neymar ambaye alimwaga wino kusaini mkataba wa miaka mitano Camp Nou 2016, ameanza maisha mapya ya Ligue 1 kwa kufunga mabao matatu na kutoa pasi ya mabao matatu zaidi katika mechi zake mbili za kwanza.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search