sPORTS nEWS: Haruna Niyonzima hatimae ametua kwa ajili ya kuzinduliwa na wana Msimbazi Simba SC siku ya 'Simba day'



Wiki iliyopita uongozi wa klabu ya Simba kupitia Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Habari wa klabu hiyo, Haji Manara ulithibitisha kuwa ni kweli umsajili Haruna Niyonzima baada ya mkataba wake na Yanga kumalizika.

Usiku wa jumapili ya Agosti, 6 mchezaji Haruna Niyonzima amewasili nchini tayari kwa ajili ya Simba Day itakayofanyika jumanne ya Agosti, 8 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo atakuwa mmoja wa wachezaji ambao watatambulishwa siku hiyo.

Pamoja na Niyonzima wachezaji wengine ambao wamewasili jumapili usiku ni Emmanuel Okwi na Nicholas Gyan.


Kaimu Makamu wa Rais wa Klabu ya Simba Iddi Kajuna akimpokea Haruna Niyonzima baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.



Credit: Mo Blog.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search