sPORTS nEWS: Singida United yapiga hodi 'bonden kwa Madiba'.. yamtwaa 'mshambuliaji kisiki' wa Kaizer Chief.. Share..
Mkurugenzi Mtendaji wa timu ya Singida United Festo Sanga (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya YARA Alexander Macedo wakibadilishana nyaraka za mkataba wa udhamini wa mwaka mmoja wenye thamani ya kiasi cha Milioni 250.
Matajiri kutoka mkoani Singida klabu ya Singida United wamefanya mabadiliko kidogo katika safu ya ushambuliaji katika usajili baada ya kufungwa na Mabingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara Yanga cha magoli 3-2 kwenye Mchezo wa Kirafiki uliochezwa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Timu hiyo iliyopanda Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu, imemchukua mshambuliaji Michelle Katsavairo kutoka klabu ya Keizer Chiefs ya Afrika Kusini kwa mkopo na kumuacha Mzimbabwe mwenzake, Wisdom Mtasa.

Mkurugenzi Mtendaji wa timu ya Singida United Festo Sanga akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utiaji saini wa makubaliano ya udhamini wa mwaka mmoja kwa timu ya Singida United wenye thamani ya kiasi cha Milioni 250.
Hayo yamethibitishwa na Mkurugenzi wa Singida United, Sanga Festo amesema kwamba baada ya kusajiliwa kwa Katsavairo kutoka Kaizer, Mtasa anapalekwa kwa mkopo wa Stand United ya Shinyanga.
Aidha Mkurugenzi huyu amesema kuwa wamefanya hivyo ili kuweza kusajili mchezaji mwingine wa kigeni japo kuwa walikuwa wamefikia idada ya wachezaji saba wa kigeni hivyo imewapelekea kumtoa mchezaji m0ja kwa mkopo.
Singida United mpaka sasa wameshacheza michezo mitano ya kirafiki wakishinda mechi mbili dhidi ya Pamba 5-0 na Alliance 2-0 huku wakitoka sare na wanajeshi wa Pwani Ruvu Shooting ya kufungana goli 1-1 na kupoteza michezo miwili dhidi ya Lipuli FC kwa kufungwa 1-0 na kufungwa 3-2 na Yanga.
Kocha Mkuu wa klabu ya Singida Hans Van Der Pluijm akiongea na waandishi wa habari baada ya Kampuni ya YARA kuingia mkataba na klabu hiyo wenye thamani ya shilingi milioni 250.
Licha ya kufungwa na Yanga ,vijana wa Hans Van Der Pluijm walicheza kandanda safi na la kuvutia na kutawala kwa kila kitu na kuwapoteza kabisa viungo wa Yanga tatizo ambalo lilitakiwa kufanyiwa marekebisho ni la golikipa na tayari timu hiyo imemsajili mlinda mlango kinda toka kwa Wekundu wa Msimbazi Simba Manyika Peter ambaye amesaini miaka miwili.

Matajiri kutoka mkoani Singida klabu ya Singida United wamefanya mabadiliko kidogo katika safu ya ushambuliaji katika usajili baada ya kufungwa na Mabingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara Yanga cha magoli 3-2 kwenye Mchezo wa Kirafiki uliochezwa uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Timu hiyo iliyopanda Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu, imemchukua mshambuliaji Michelle Katsavairo kutoka klabu ya Keizer Chiefs ya Afrika Kusini kwa mkopo na kumuacha Mzimbabwe mwenzake, Wisdom Mtasa.
Mkurugenzi Mtendaji wa timu ya Singida United Festo Sanga akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utiaji saini wa makubaliano ya udhamini wa mwaka mmoja kwa timu ya Singida United wenye thamani ya kiasi cha Milioni 250.
Hayo yamethibitishwa na Mkurugenzi wa Singida United, Sanga Festo amesema kwamba baada ya kusajiliwa kwa Katsavairo kutoka Kaizer, Mtasa anapalekwa kwa mkopo wa Stand United ya Shinyanga.
Aidha Mkurugenzi huyu amesema kuwa wamefanya hivyo ili kuweza kusajili mchezaji mwingine wa kigeni japo kuwa walikuwa wamefikia idada ya wachezaji saba wa kigeni hivyo imewapelekea kumtoa mchezaji m0ja kwa mkopo.
Singida United mpaka sasa wameshacheza michezo mitano ya kirafiki wakishinda mechi mbili dhidi ya Pamba 5-0 na Alliance 2-0 huku wakitoka sare na wanajeshi wa Pwani Ruvu Shooting ya kufungana goli 1-1 na kupoteza michezo miwili dhidi ya Lipuli FC kwa kufungwa 1-0 na kufungwa 3-2 na Yanga.
Kocha Mkuu wa klabu ya Singida Hans Van Der Pluijm akiongea na waandishi wa habari baada ya Kampuni ya YARA kuingia mkataba na klabu hiyo wenye thamani ya shilingi milioni 250.
Licha ya kufungwa na Yanga ,vijana wa Hans Van Der Pluijm walicheza kandanda safi na la kuvutia na kutawala kwa kila kitu na kuwapoteza kabisa viungo wa Yanga tatizo ambalo lilitakiwa kufanyiwa marekebisho ni la golikipa na tayari timu hiyo imemsajili mlinda mlango kinda toka kwa Wekundu wa Msimbazi Simba Manyika Peter ambaye amesaini miaka miwili.
Mkurugenzi Mtendaji wa timu ya Singida United Festo Sanga (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya YARA Alexander Macedo wakitia saini karatasi ya makubaliano ya udhamini wa timu ya Singida wenye thamani ya Milioni 250.
Singida United itatumia uwanja wake wa nyumbani wa Jamhuri Dodoma kutokana na uwanja wa Namfua bado upo katika matengenezo makubwa na utakapokamilika timu hiyo itaweza kurejea katika makazi yake na inatazamiwa kuleta changamoto kubwa kwa timu kubwa kutokana na kufanya usajili mkubwa huku ikiwa ndio kinara kwa kuwa na wadhamini wengi kuliko timu yoyote ile Tanzania tangu lingi ianzishwe.
Singida United itatumia uwanja wake wa nyumbani wa Jamhuri Dodoma kutokana na uwanja wa Namfua bado upo katika matengenezo makubwa na utakapokamilika timu hiyo itaweza kurejea katika makazi yake na inatazamiwa kuleta changamoto kubwa kwa timu kubwa kutokana na kufanya usajili mkubwa huku ikiwa ndio kinara kwa kuwa na wadhamini wengi kuliko timu yoyote ile Tanzania tangu lingi ianzishwe.
No comments:
Post a Comment