sPORTS nEWS: Hazard, Kante, Sanchez na Kane kuchuana na Messi, Ronaldo kugombea uchezaji bora FIFA...#share
Harry Kane, Eden Hazard, N'Golo
Kante and Alexis Sanchez wametajwa katika orodha ya wachezaji wanaowania zawadi
ya mchezaji bora wa Dunia.
Wachezaji hao wa klabu ya Chelsea Eden Hazard na N’Golo Kante
na Mshambuliaji wa Tothenham Harry Kane n mshambuliaji wa klabu ya Arsenal
wameorodheshwa katika orodha ya wachezaji wanaowania mchezaji bora wa kiume wa
FIFA kwa mwaka 2017.
Wachezaji hao wanaungana na wachezaji na Lionel Messi,
Cristiano Ronaldo, Zlatan Ibrahimovic and Neymar katia orodha ya wachezaji 24
ambapo mshindi atatangazwa mwezi Januari.
Eden Hazard amekuwa amewekwa katika orodha hiyo kutokana na kufanikiwa
kufunga magoli 16 na kufanya vizuri ndani ya jezi ya Chelsea na kuisaidia
kupata ubingwa msimu uliopita.
Huku mchezaji mwenzake Kante, pia akichangia kwa kiasi kikubwa
mafanikio ya Chelsea mwaka mmoja baada ya kufanya hivyo akiwa na klabu ya Leicester
kwa kuchukua ubingwa wa ligi ya Uingereza.
Mshambuliaji wa Totteniham Harry Kane amefika hapo kwa
kufanya vizuri msimu uliopita kwani alifunga magoli 29 na kuisaidia klabu yake kushika nafasi ya
pili katika msimamo wa ligi lakini pia ndiye mchezaji aliyechukua kiatu cha
dhahabu.
Wakati Sanchez, alimaliza msimu wa 2016-17 kwa kuchukua ubingwa wa FA, lakini pia laifanikiwa kufunga magoli 24.
The Fifa Best Men's Player 2017 shortlist
Pierre-Emerick Aubameyang, Leonardo Bonucci, Gianluigi
Buffon, Dani Carvajal, Cristiano Ronaldo, Paulo Dybala, Antoine Griezmann, Eden
Hazard, Zlatan Ibrahimovic, Andres Iniesta, Harry Kane, N'Golo
Kante, Toni Kroos, Robert Lewandowski, Marcelo, Lionel Messi, Luka Modric,
Keylor Navas, Manuel Neuer, Neymar, Alexis Sanchez, Luis Suarez,
Arturo Vidal.
No comments:
Post a Comment