tETESI zA uSAJILI uLAYA: Martial aichomolea Inter Milan, ataka kubaki kwa Malkia...#share

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Manchester
United Anthony Martial amekataa kujiunga na klabu ya Inter Milan, mshambuliaji
huyo anataka kubaki katika ligi ya Uingereza (Premier stay).
Inter imeulizia mshambuliaji huyo wa Kifaransa kuwa sehemu ya
dili la uhamisho wa Ivan Perisic kwenda Manchester United.
Klabu hiyo ya San Siro
imehitaji kiasi cha sh. £48m pamoja na
Martial kwa mkopo lakini kwa sasa inadaiwa kuwa mchezaji mwenyewe hataki
kuhamia ligi ya Serie A.
Mwandishi wa habari wa Italian Tancredi Palmeri ameandika
kwenye ukurasa wake wa Twitter: “Martialkwa sasa amekataa pendekezo la Inter. Anependelea
kubaki katika Premier kama inawezekana,”.
Licha ya kwamba Martial hayupo tayari kwa uhamisho huo,
Perisic anaweza kukamilisha uhamisho wake kwenda Old Trafford.
Inter na United wamekuwa katika misuguano ya kukubaliana ada
ya uhamisho ya Mkoreshia huyo tangu suala hilo lianze kuzungumzwa miezi kadhaa
sasa.
Inaarifiwa kuwa mwishoni mwa wiki iliyopita Ed Woodwood
alifungua mazungumza ya uhamisho wa Perisic kwa kiasi cha £48m.
No comments:
Post a Comment