Wanachama TEF nako 'washikana mashati' walaani maamuzi ya Viongozi wao kuondosha 'marukufuku' kwa RC Makonda 'kinyemela'.. #share
WANACHAMA
wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), wametoa onyo kwa uongozi wa jukwaa hilo
kwa kitendo cha kutoa uamuzi wa kuandikwa na vyombo vya habari taarifa
za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam bila kuwashirikisha.
Onyo
hilo limetolewa kupitia katika taarifa yake kupitia kwa Mwenyekiti wa Kamati
Maalum ya Mkutano Mkuu Maalum wa TEF, Walles Maugo kwa niaba ya wajumbe wa
jukwaa hilo baada ya kikao cha dharura kilichofanyika mwishoni mwa wiki jijini
Dar es Salaam.
Maugo
amesema baada ya wajumbe kukutana na kujadili walibaini kuwepo kwa kasoro kubwa
wakati wa mchakato wa kurejesha uhusiano wa kikazi kati vyombo vya habari na
mkuu huyo wa mkoa.
Amesema
jukwaa kwa kauli moja limeutaka uongozi kutorudia tena kosa hilo la
kiuwajibikaji, kikanuni na kitaratibu.
“Pia
uongozi umetakiwa kuhakikisha kila panapotokea suala kama hilo ambalo
lilifanyiwa uamuzi na mkutano mkuu wa TEF kwa kushirikiana na taasisi nyingine
za kihabari, unarejeshaje kwa wanachama kabla ya hatia za mwisho kuchukuliwa,”
alisema
Amesema
viongozi wa TEF ambao walitoa maamuzi hayo walikiri kosa na kuomba radhi kwa
kuitisha mkutano wa waandishi wa habari kabla ya kupata idhini ya mkutano mkuu
hali ambayo inajenga taswira mbaya ya kiuwajibikaji kwa jukwaa.
Maugo
amesema TEF inawahakikishia wanahabari na wananchi kuwa litaendelea kutimiza
wajibu wake wa kitaaluma na halitasita kuchukua hatua stahiki kwa kiongozi au
mtu yeyote atakayeonekana kutishia usalama wa wanahabari, uhuru wa uhariri na
vyombo vya habari.
Na Mwandishi Wetu
No comments:
Post a Comment