Baada ya Kubenea, Zitto, na Lema, Spika Ndugai aingia 18 za Peter Msigwa.....#share

MBUNGE wa Iringa Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Peter Msigwa amesema Spika Job Ndugai hana sifa ya kuwa kiongozi wa kusimamia nidhamu ndani ya bunge.


Msigwa amebainisha hayo leo jijini Nairobi nchini Kenya  alipokwenda kwa ajili ya kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chadema  Tundu Lissu aliyelazwa kufuatia shambulio la kupigwa risasi na watu wasiojulikana.

Itakumbukwa hivi karibuni Lissu alipigwa risasi zaidi ya 30 akiwa mjini Dododoma kwa ajili ya mikutano ya Bunge inayoendelea hali iliyopelekea kusafirishwa kwa matibabu nchini Kenya.

"Ninaomba mumuogope Mungu kwa sababu tunaleta mchezo na maisha ya Watanzania, mnataka kutunyamazisha ili tusiseme. Tutasema mpaka mwisho wetu kwa sababu uhai wetu na usalama wa taifa letu umetishiwiwa kwa kiwango cha juu sana lakini Mhe.

Ndugai wewe kama spika unasifa gani ya kutuambia sisi tuwe na adabu ndani ya bunge wakati wewe mwenyewe kipindi cha kampeni ulionekanaa ukipiga watu hadharani na fimbo, ulitakiwa uwe gerezani na siyo kutusimamia nidhamu ndani ya bunge", amesema Msingwa.

Aidha amedai kuwa Ndugai ni adui wa usalama wa Taifa nchini kutokana na kulisababisha bunge kuwa dhaifu kwani serikali imemteka kiasi cha kupokea maagizo toka serikalini hivyo kuufanya mhimili wa bunge kuwa butu na kushindwa kuisimamia.

“Nasema haya kwa ujasiri mkubwa sina kitu cha kuogopa tena kama ndugu yetu ameshapigwa risasi na tumeshaambiwa tunaofutwa ni sisi hivyo hatuna cha kuogopa kusema jambo lolote", amesisitiza Msigwa.

Pia Mbunge huyo  ameongeza kutokana na tabia za Spika huyo wakati mwingine  wanashindwa hata kuwaambia watoto wao kuwa ni kiongozi wao wa bunge kwani mekuwa wakiwatishwa, wakifukuzwaa paoja pamoja na kupigwa pingu huku akisisitiza kuwa yupo tayari kufukuzwa bungeni lakini hatoweza kukaa kimya.

Na Abrahama Ntambara


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search