Benki ya Afrika-Tanzania yazindua huduma ya 'SWAHIBA Mobile App' kurahisisha huduma za kibenki...#share

BENKI ya Afrika-Tanzania (BOA) imezindua programu ya benki inayoitwa ‘SWAHIBA Mobile App’ ambayo itawawezesha watumiaji wa Banki hiyo kufurahia huduma kamili za benki kwa njia ya simu  kupitia mtandao wowote wa simu muda wote.

Vingozi wa BOA wakifurahia jambo baada ya uzinduzi wa huduma ya 'SWAHIBAMobile App' leo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini leo Dar es Salaam, Mkuu wa Kitengo cha Huduma za E-Banking wa benki hiyo Emmanuel Mshindo, amesema programu hiyo itawarahisishia wateja  kutumia huduma za kibenki katika simu kwani inasifa zinazowapa wateja uwezo wa kufikia zao binafsi na za kibiashara kwa wakati mmoja.

“Huduma zinazopatikana kwenye program hii ni huduma za kuhamisha fedha, huduma za hundi, maombi ya mkopo wa papo hapo, malipo ya bili, huduma za utoaji fedha kwenye ATM bila kadi, kuongeza muda wa maongezi, usajili binafsi wa mobile banking na huduma za e-chama pamoja na nyingine nyingi,” amesema Mshindo.

Aidha amesema zaidi ya hayo, SWAHIBA Mobile App itakuwa na uwezo wa kutumiwa na mtu yeyote hata ambaye siyo mteja wa benki hiyo. Ametaja huduma ambazo mteja mwingine anaweza kupata ni huduma za Bank Of Africa, Maombi ya Mikopo, Matawi ya benki na ATM, benki katika mtandao ‘internent banking’ na viwango vya ubadilishaji fedha za kigeni.



Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa BOA, Ammishaddai Awusu-Amoah, amesema wanajivunia kuanzisha program hiyo ya benki kiganjani katika wakati huu ambapo benki yao inaadhimisha miaka 10 ya biashara nchini.

“Uzinduzi wa SWAHIBA Mobile App ni alama ya shukrani zetu kwa wateja, jamii na wadau wote katika kipindi cha miaka 10 ya kazi nchini,” amesema.

“Huduma hii pia inakuja kutia msisitizo wa ahadi yetu ya kuweka mapendekezo ya wateja wetu kwanza na kuwaongezea uzoefu wa kidigitali zaidi katika ukuaji wa sayansi na teknolojia. Pia inathibitisha uamuzi wa benki wa kujenga uwepo wake wa kidigitali na kukidhi mahitaji ya haraka ya wateja wetu,” ameongeza Awusu-Amoah.



Kwa upande wake Mkurugenzi wa Maxcom Afrika Jimson Kasatti amesema huduma hiyo pia inapatikana kupitia Max Malipo na kuongeza kuwa wapo mbioni kujiunga na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) ili kuwa wezesha wananchi kununua na kumiliki hisa kutoka Max Malipo.





Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search