Baada ya Spika Ndungai, Lema 'amuamshia dude' Humphrey Polepole,.. asema tamko la kumpongeza'Turky' ni la (...) #share

BAADA ya juzi Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kumshambulia Spika wa Bunge Job Ndugai kuwa anapotoha juu ya taarifa za matibabu ya Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)  Tundu Lissu

Lakini pia kwa kushindwa kulisimamia Bunge wakati huu ambao Lissu yuko jijini Nairobi nchini Kenya kwa matibabu. 

Mbunge huyo amegeuzia mashambulizi kwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole kwa kumwambia kuwa ametoa tamko la kijinga. 
"Humphrey Polepole,  nimeona tamko la kijinga lililojaa uongo. Hata hivyo linafanana na wasi wasi wa fikra zako," amesema Lema kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Aidha shambulizi hili la lema dhidi ya Polepole limekuja baada ya Polepole kumpongeza Mbunge wa Mpendae CCM kukisaidia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)  kukodi ndege iliyomsafirisha Kiasi kwa ajili ya matibabu. 

"Tanzania ni moja,  ni nchi yetu sote, na itajengwa na wazalendo, wenye utu,  mshikamano na upendo. Tutende wema,  hongera Mwana CCM Mr.  Wote, " amesema Polepole kwenye ukurasa wake wa Twitter.  
 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search