Breaking: ACACIA 'yapumulia mashine' kwa sababu ya makinikia.. BOFYA hapa uone walichokiamua jioni hii kuhusu mgodi wao wa Bulyanhulu.. #share
KAMPUNI ya Acacia imetangaza lengo lake la kupunguza shughuli
za uendeshaji na uzalishaji katika Mgodi wa Bulyanhulu kutokana na upungufu wa
mzunguko wa pesa uliosababishwa na zuio la usafirishaji wa makinikia kwenda nje
ya nchi na mazingira ya uendeshaji kuwa magumu.
Tangu zuio la mchanga wa dhahabu na shaba liwekwe na Serikali
mnamo Machi 3, 2017 na kuathiri takribani 35% ya uzalishaji wa mwaka, Acacia
imekuwa na takribani mchanga wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 265
ndani ya nchi kulingana na bei za sasa
Katika kusaidia kukabili hasara hizi, Acacia imeamua kuchukua
hatua kadhaa ikiwemo kupunguza uzalishaji katika mgodi wa Bulyanhulu ili
kulinda ajira za wafanyakazi na watoa huduma mgodini ambao ni Watanzania.
Kampuni ya Acacia bado ina matumaini katika majadiliano
yanayoendelea kati ya Barrick na serikali ikiamini yatapelekea muafaka juu ya
zuio la makinikia na mazingira ya uendeshaji yatakayowezesha tathmini mpya ya
hali ya uendeshaji kwa siku zijazo.






No comments:
Post a Comment