Breaking: ACACIA 'yapumulia mashine' kwa sababu ya makinikia.. BOFYA hapa uone walichokiamua jioni hii kuhusu mgodi wao wa Bulyanhulu.. #share


KAMPUNI ya Acacia imetangaza lengo lake la kupunguza shughuli za uendeshaji na uzalishaji katika Mgodi wa Bulyanhulu kutokana na upungufu wa mzunguko wa pesa uliosababishwa na zuio la usafirishaji wa makinikia kwenda nje ya nchi na mazingira ya uendeshaji kuwa magumu.

Tangu zuio la mchanga wa dhahabu na shaba liwekwe na Serikali mnamo Machi 3, 2017 na kuathiri takribani 35% ya uzalishaji wa mwaka, Acacia imekuwa na takribani mchanga wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 265 ndani ya nchi kulingana na bei za sasa

Katika kusaidia kukabili hasara hizi, Acacia imeamua kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kupunguza uzalishaji katika mgodi wa Bulyanhulu ili kulinda ajira za wafanyakazi na watoa huduma mgodini ambao ni Watanzania.


Kampuni ya Acacia bado ina matumaini katika majadiliano yanayoendelea kati ya Barrick na serikali ikiamini yatapelekea muafaka juu ya zuio la makinikia na mazingira ya uendeshaji yatakayowezesha tathmini mpya ya hali ya uendeshaji kwa siku zijazo.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search