Breaking: Mbunge Zitto Kabwe Anashikiliwa na Jeshi la Polisi....Taarifa na Matukio360..#share

KIONGOZI wa Chama cha ACT Wazalendo, na Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe amekamatwa na Polisi muda huu uwanj a wa ndege wa wa Julius Nyerere (JNIA),jijini Dar es salaam wakati akitoka Kigoma.


Kwamujibu wa Afisa habari wa chama hicho Abdallah Khamisi amesema Kwa sasa wanasheria wa chama wanafuatilia kujua sababu za kukamatwa kwake.


Mbunge Zitto amekamatwa kufuatia agizo la Katibu Mkuu wa Bunge Dk. Thomas Kashililah ambaye jana aliagiza Mbunge huyo asakwe popote alipo ili apelekwe kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge.


Aidha kwa mujibu wa Dk. Kashililah ni kwamba Zitto alikwishapatiwa barua ya kutakiwa kufika mbele ya Kamati hiyo lakini hakufanya hivyo.

Itakumbukwa pia jana Mbunge wa Ubungo Sued Kubenea alikamatwa na Jeshi la Polisi na kisha leo Alfajiri akasafirishwa kenda mjini Dodoma.

No automatic alt text available.
Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search