Bavicha Watangaza Maandamano...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360...#share

BARAZA la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha) Mkoa wa Kagera limetangaza kuandaa maandamano ya amani kulaani tukio la kushambuliwa kwa risasi Mwanasheria Mkuu wa chama chao, Tundu  Lissu  aliyeshambuliwa Septemba 7, mwaka huu.
Image result for bavicha
Mwenyekiti wa Bavicha Manispaa ya Bukoba,  Ishengoma Audax alisema licha ya kuandamana watakwenda katika Hospitali ya Rufaa Bukoba kuchangia damu.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Kagera, Francis Rutta amesema wameamua kuandamana kulaani kushambuliwa kwa Lissu na kuvitaka vyombo vya dola kuhakikisha vinawakamata na kuwatia mbaroni wahusika.

“Tunafanya maandamano ya amani hivyo hatutegemei polisi kuzuia maandamano yetu kwa kuwa ni ya amani.      
“Lakini tunaunga mkono uamuzi wa Brlaza Kuu la Taifa Bavicha linaloongozwa na Mwenyekiti Patrobas Katambi,” amesema.

Amesema wamekuwa wakishangazwa na hatua ya polisi kuwazuia wananchi kumuombea Tundu Lissu ikiwa ni pamoja na kukamatwa kwa makada wa chama chao waliovaa fulana zenye ujumbe wa kumuombea.


Amesema  huo ni ukiukaji mkubwa wa demokrasia.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search