bREAKING nEWS: Chadema yatoa 5 kwa Mahakama Kenya kufuta ushindi wa Kenyatta, Pia yashauri mambo 3 kufanyika nchini ili kuiga nyendo za Kenya...#share

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mahakama ya Juu ya Kenya (The Supreme Court of Kenya) imeweka historia Afrika. Baada ya kushuhudia Mahakama ikiendeshwa kwa uhuru na uwazi huku ikitangazwa moja kwa moja na vyombo vya habari vya nje na ndani ya Kenya.


Leo imehitimisha kesi kwa kutoa hukumu ya kihistoria na ambayo imeweka funzo kubwa na muhimu katika ukuaji na uimarishaji wa demokrasia katika Bara la Afrika.

Mahakama ya Juu ya Kenya imeagiza uchaguzi wa Rais ufanyike upya ndani ya siku 60 kama ambavyo Katiba ya Kenya inataka.

Hukumu hii imetolewa kutokana na uhuru wa Mahakama ya Kenya ambao umetokana na misingi iliyowekwa na Katiba na Sheria za nchi hiyo.

Kutokana na historia hiyo ya kipekee iliyoandikwa na majirani zetu wa Kenya kupitia Mahakama ya Juu, CHADEMA tunashauri ifuatavyo;

1. Ni wakati mwafaka sasa Tanzania tukarejea katika mchakato wa kupata Katiba Mpya na yenye kuweka taasisi imara.

2. Rais John Magufuli amdhibitishe Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania kwani hadi sasa amekaa muda mrefu akikaimu tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo. Hii itasaidia kuufanya mhimili huu uweze kuwa huru na kujisimamia katika shughuli zake za kutafsiri sheria na kutoa haki.

3. Katiba Mpya ambayo Watanzania wanaitaka iweke kipengele cha matokeo ya urais baada ya uchaguzi mkuu, kuhojiwa mahakamani.

4. Katiba Mpya iunde Tume Huru ya Uchaguzi na ambayo pia itaweza kushtakiwa mahakamani pale ambapo kuna tuhuma au madai ya uchaguzi kuharibiwa au kuingiliwa kinyume cha taratibu za uchaguzi huru na haki.

Hukumu ya Mahakama ya Juu ya Kenya ituamshe Watanzania kwa pamoja tudai Katiba mpya na ambayo itaweka misingi imara ya taasisi zetu nchini na hatimaye tuweze kuwa na chaguzi huru na za haki.

Mwisho tunawatakia Wakenya uchaguzi mwema wa marudio baada ya hukumu hiyo ya kihistoria ambayo imedhihirisha uimara mkubwa wa demokrasia na utawala bora.

Hiyo ni ishara na funzo kubwa linaloonesha ukomavu wa taasisi zilizoundwa kikatiba.

Imetolewa leo Ijumaa, Septemba 01 Septemba 2017.
John Mrema

Mkurugenzi wa Itifaki, Uenezi, Mawasiliano na Mambo ya Nje

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search