sPORTS nEWS: Mshambuliaji wa Everton Wayne Rooney ashikiliwa na Jeshi la polisi wa kosa la kuendesha.....#share


NAHODHA wa Zamani wa Timu ya Taifa ya Uingereza Wayne Rooney anashikiliwa na jeshi la Polisi nchini humo akiwa karibu na nyumbani kwake katika mji wa Cheshire kwa kosa la kuendesha gari huku akiwa amelewa.




Kwa mujibu wa the Mirror, Rooney ambaye ni Mfungaji bora wa muda wote wa Uingereza amekatwa usiku wa jana alipokuwa katika mtoko wake wa jioni

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 inaaminika kuwa alipelekwa katika kituo kiudogo cha polisi kilichopo kwenye mji wa Cheshire ambapo alihojiwa na maofisa  wa polisi.


Chanzo kinasema kuwa : 'Maongezi yake yalikuwa hayaeleweki, mdomo wake ulikuwa mwekundu na wine pamoja na macho yeke kuwa mekundu.

Tangu ajiunge tena na klabu ya Everton Rooney amefunga magoli 2 katika michezo mitatu na alicheza pia katika mchezo ambao klabu yake ilipoteza 2-0 dhidi ya Chelsea.

Rooney siyo mchezaji wa kwanza wa kimataifa kusimamishwa na kukamatwa na polisi kwa kusa la kuendesha gari huku amelewa.  

Mwezi wapili mwaka huu mshambuliaji wa klabu ya Liverpool  Roberto Firmino alifungiwa kuingia barabarni kwa mwaka mmoja na kupigwa faini ya pauni Milioni 20,000 kwa kosa la jinsi hiyo.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search