Breaking: Tundu Lissu 'kutwaa shavu' Marekani.. atajwa kuwa 'Mwafrika wa kwanza' kufanya hivyo katika miaka ya hivi karibuni.. Hongera Sana Lissu.. #share
HATIMAYE nyota ya Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama cha Wanasheria nchini (TLS),Tundu Lissu imeanza kung’aa katika anga za kimataifa baada ya Gwiji huyo wa sheria nchini kupata Mwaliko kwenye Mkutano mkubwa wa sheria Duniani.
Tundu Lissu ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema amepata Mwaliko katika Mkutano wa Mawikili Bingwa wa Sheria Nchini Marekani.
Mkutano hao unatarajiwa kuhudhuliwa na mawakili Bingwa kutoka Nchi tofauti Duniani utarajia kufanyika Jiji la Washington Dc siku ya Ijumaa ya tarehe 15/09/2017.
Katika Mkutano huo, Lissu anatajwa kuwa ni Mwafrika wa kwanza kuhudhulia ikitajwa sababu kuu kwa Gwiji huyo wa sheria kupewa mwaliko kwenye mkutano huo kuwa ni kutokana na Umahiri wake wa sheria pamoja na kujitokeza kuwatetea wanyonge kupitia sheria.
No comments:
Post a Comment