Jeshi la Polisi nchini Latoa Onyo Kwa Wahalifu wa Mtandaoni...#share

JESHI la Polisi nchini limesema limejipanga vyema kupambana na viotendo vya uhalifu wa mitandaoni huku likibainisha kuwa vitendo hivyo vimepungua kwa mwaka huu ukilinganisha na mwaka jana.





Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Msemaji wa jeshi hilo Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Barnabas Mwakalukwa, wakitoa taarifa ya hali ya makosa ya kimtandao yalivyo kwa hivi sasa, amesema kuundwa kwa Sheria ya Makosa ya Mtandao imesaidia kupunguza uhalifu huo.

Akitaja takwimu za makosa hayo kwa mwaka jana amesema uhalifu wa kupitia ATM, makosa yaliyolipotiwa ni 260 , wizi kwa njia ya simu matukio 3233, lugha ya matusi matukio 911, matukio ya uchochezi 115 kutishia kuua 1210, vitisho vya kawaida 317.

“Lakini ukilinganisha mwaka huu kuanzia Januari hadi Septemba matukio ya uhalifu yapo 1663 na ni kwamba lugha ya matusi yako matukio 327, lakini kutishia kuua ni matukio 304, utapeli 36 na kuna kesi ambazo zimelipotiwa,” amesema ASP Mwakalukwa.

Akifafanua kuhusu kesi zilizoripotiwa ni kwamba mwaka jana zulikuwa 573 ukilinganisha na mwaka huu wenye kesi 553. Pia watuhumiwa waliokamatwa mwaka jana ni 1080 ukilinganisha na watuhumiwa 315 kwa mwaka huu huku waliopelelezwa na kutiwa hatiani kwa mwaka uliopita walikuwa  watu 88 wakati mwaka huu 19.

ASP Mwakalukwa amewataka wananchi wanapokumbwa na uhalifu wa jinsi hiyo kuripoti kituo cha polisi badala ya kuzungumza na vyambo vya habari kwani wataharibu uchunguzi wao.

Kaimu Mkurugenzi wa Masuala ya Watumiaji na Watoa Huduma za Mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Thadeo Ringo amesema changamoto kubwa za kihalifu wanazokumbana nazo ni mbili, upotevu wa fedha kwa njia ya simu na ATM.

Amesema kwa njia ya simu ni kwamba mara nyingi watu wamekuwa wakikosea namba wanapotuma fedha kwani wamekuwa wakikosea namba na kutuma kwa mtu ambaye si mlengwa. Kutokana na hali hiyo aliwataka wananchi kabla ya kutuma fedha kujiridhisha kwanzakama unayetaka kumtumia ndiye.


Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search