Kenya: Raila Odinga 'aamsha farasi' jijini Nairobi na kusema 'hatuitaki Tume hii ya Uchaguzi..' #share

Umoja wa muungano wa vyama vya upinzani nchini Kenya NASA, umedai kutaka mabadiliko yafanyike ndani ya Tume ya Uchaguzi na Mipaka, IEBC, kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mpya wa urais.
Kiongozi wa umoja huo wa upinzani, Raila Odinga, amesema Tume ya Uchaguzi haiaminiki na haiwezi kusimamia Uchaguzi utakaokuwa huru na haki kama Mahakama Kuu ilivyoagiza.
Kauli ya Odinga imekuja baada ya kuanza kwa kampeni yake ya kwanza jijini Nairobi leo kutokana na uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Juu Ijumaa iliyopita ambapo ilibatilisha matokeo ya ushindi wa Uhuru Kenyatta .
Pamoja na hayo Odinga amekosoa kauli ya Rais Kenyatta ya kuwashtumu Majaji kwa kudai kuwa upinzani hawataki uchaguzi lakini wanataka serikali ya muungano, madai ambayo Odinga amepuuzilia mbali na kusema hawawezi kushirikiana na wezi wa kura.
Kenya inaelekea kwenye Uchaguzi mpya ndani ya siku 60 baada ya Mahakama ya Juu nchini humo kufuta ushindi wa rais Uhuru Kenyatta kwa kubaini kuwa, haukuwa wa huru na haki.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search