sPORTS nEWS: Mchakato wa Bilionea MO Dewji kumilikishwa Simba hatua za mwisho kukamilika..Kamati maalumu yatangazwa leo kusimamia mchakato huo....#share

KATIKA kile ambacho tunaweza kusema kwamba ni hatua za mwisho mwisho kwa klabu ya Simba kukamilisha mchakato wa kumilikiwa kwa mfumo wa hisa. Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo leo imetangaza kamati maalumu ya kusimamia mchakato wa zabuni wa kumpata mwekezaji katika mfumo huo.


Katika mfumo huo mpya asilimia 50 ya kampuni itakayoanzishwa, itatolewa kwa mwekezaji/wawekezaji atakayetokana miongoni mwa wanachama wa Simba SC kupitia mchakato wa zabuni.

Kamati hiyo maalumu iliyotangazwa itaongozwa na Jaji Msataafu wa Mahakama Kuu Thomas Mihayo kama Mwenyekiti samaba na wajumbe wanne ambao ni Mussa Azzan Zungu, Abdulrazaq Badru ambaye ni Mkurugenzi wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu nchini, Wakili Damas Ndumbaro na Yusuph Maggid Nassoro.


Na Abraham Ntambara

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search