Kubenea adai Tundu Lissu anawajua waliompiga risasi.. #share


MBUNGE wa Ubungo, Saed Kubenea ameeleza kuwa Tundu Lissu amesema kwamba anawajua waliompiga risasi na kama Jeshi la Polisi litawakamata anaweza kuwatambua kwa sura.

Aidha, Kubenea amedai kuwa Tundu Lissu amesema washambuliaji hao walianza kumfuatilia kuanzia Tegeta-Dar na baada ya kugundua anafuatiliwa aliweza kuwakimbia hadi Dodoma na kuwaacha.

Kubenea ameyasema maneno hayo mapema leo alipopewa nafasi ya Kusalimia katika ibada iliyofanyika kwenye kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo Ubungo jijini Dar Es Salaam.

Na Mwandishi Wetu


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search