Mahakamani Kisutu: Mholanzi Adai Kuchaniwa Pasport Yake na Polisi...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360..#share


RAIA wa Uholanzi Monique Amanzi mwenye (28) ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Septemba 22, 2017 kuwa alichaniwa Passport yake na Ofisa wa Polisi Kitengo cha Usalama Barabarani (Trafiki).

Mholanzi huyo anakabiliwa na tuhuma za kuishi nchini bila kibali.

Amanzi ambaye pia anahusishwa na biashara ya kujiuza, alisomewa kosa lake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa na Wakili wa Uhamiaji Novatus Mlay ambapo Wakili huyo alidai kuwa September 11, 2017 Idara ya Uhamiaji Makao Makuu, Kurasini Temeke ilimbaini kuwa anaisha nchini kinyume na sheria.

Baada ya kusomewa Amanzi alikana kosa, ambapo alidai kuwa rafiki yake wa kiume ambaye ni Polisi Kitengo cha Usalama wa Barabarani anayefanya kazi maeneo ya Victoria Makumbusho alichana hati yake ya kusafiria akidai baada ya kuchanwa kwa hati hiyo aliripoti Polisi Kinondoni miaka miwili iliyopita lakini alipoteza RB na kwamba ana watoto watatu ambapo mmoja amefariki.

Miongoni mwa watoto hao wawili ni wa mume wake Ibrahimu Abas ambaye alikuja nae hapa nchi lakini walitengana na kumpata Trafiki ambaye alizaa naye mtoto mmoja bahati mbaya akafariki.

Alidai kuwa aliwahi kwenda Uhamiaji lakini hakupata mafanikio.

Dhamana ya mshtakiwa iko wazi ambapo anatakiwa kuwa na wadhamini wawili raia wa Tanzania ambao kila mmoja atasaini bondi ya Tsh Milion Moja ambapo hata hivyo, upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na Hakimu Nongwa aliahirisha kesi hadi Septemba 27, 2017 kwa ajili ya kutajwa.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search