Mbunge CCM atoa ufafanuzi sababu ya kukodi ndege ya Lissu kwenda matibabu Nairobi, Kenya...#share
MBUNGE wa Mpendae kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Salim Hassan Turky amesema Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema) kumemlipa fedha alizowadhamini ili kufanikisha
ukodishwaji wa ndege iliyomsafirisha
Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) Tundu Lissu kwenda jijini
Nairobi nchini Kenya kwa matibabu baada ya kupigwa risasa akitokea Mkoani
Dododoma.

Ametoa ufafanuzi huo leo kutokana na Kauli iliyotolewa na
Spika wa Bunge Job Ndugai kwamba Turky ndiye aliye gharamia fedha za ndege
jambo ambalo lilipingwa na chadema na kudai kuwa anapotosha umma.
Aidha Turky amesema kuwa aliamua kufadhili fedha hizo
kutokana na kwamba hawakuwa na fedha taslimu za kuweza kulipia ndege.
“Tusifanye tukio la Tundu Lissu kuwa la siasa. Mimi binafsi
tukio zima la mbunge mwenzangu limenisikitisha sana limenisononesha sana.
Nikiwa kama kamishna wa Bunge lakini pia ni binadamu kuna kuzaliwa na
kufa,”amesema.
“Kwa hiyo tukio hilo lilipotokea tuliitwa na makamishna wote na Spika wetu wakiwemo Mbowe (Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani) Msigwa na timu yake. Kwanza ndege ilikuwepo pale Airport ambayo ilikuwa imeshaagizwa na Bunge iko stand by kumpeleka moja kwa moja Muhimbili.”
Amesema walichoamua ni kuwa aende moja kwa moja Nairobi nchini Kenya lakini ndege hiyo haikuwa na kibali cha kwenda nchini humo na kwamba ili uweze kwenda nchini humo unalazimika kuwa na marubani wawili.
Hata hivyo, amesema Spika Ndugai alihangaika kupata kibali cha ndege iliyokuwepo uwanjani ili iweze kumpeleka mgonjwa Nairobi.
“Wakati mambo yote tayari rubani wa ndege akasema kuna kitu kinaitwa landing Instrument ambayo ile ndege haina kwa hiyo haitaweza kuruka,” amesema.
Amesema kutokana na majibu hayo waliingiwa na sitofahamu watafanya nini lakini yeye aliingia katika uzoefu wake aliopewa na Mungu kwa kutafuta ndege kwa ndugu zake ambao wanafanya nao biashara sana.
“Nikawaambia ndege ipo wakatoa nauli zao za ghali ghali kwa sababu tunajuana wakakubali kutusaidia kwa dola 9,200 pamoja na ambulance (gari la wagonjwa) mimi ndio niliyoita kwa kubaliana na Mbowe na Msigwa kwamba Turky haya mambo yasimamie baadaye…na ndicho kilichofanyika,” amesema.
“Kwa hiyo tukio hilo lilipotokea tuliitwa na makamishna wote na Spika wetu wakiwemo Mbowe (Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani) Msigwa na timu yake. Kwanza ndege ilikuwepo pale Airport ambayo ilikuwa imeshaagizwa na Bunge iko stand by kumpeleka moja kwa moja Muhimbili.”
Amesema walichoamua ni kuwa aende moja kwa moja Nairobi nchini Kenya lakini ndege hiyo haikuwa na kibali cha kwenda nchini humo na kwamba ili uweze kwenda nchini humo unalazimika kuwa na marubani wawili.
Hata hivyo, amesema Spika Ndugai alihangaika kupata kibali cha ndege iliyokuwepo uwanjani ili iweze kumpeleka mgonjwa Nairobi.
“Wakati mambo yote tayari rubani wa ndege akasema kuna kitu kinaitwa landing Instrument ambayo ile ndege haina kwa hiyo haitaweza kuruka,” amesema.
Amesema kutokana na majibu hayo waliingiwa na sitofahamu watafanya nini lakini yeye aliingia katika uzoefu wake aliopewa na Mungu kwa kutafuta ndege kwa ndugu zake ambao wanafanya nao biashara sana.
“Nikawaambia ndege ipo wakatoa nauli zao za ghali ghali kwa sababu tunajuana wakakubali kutusaidia kwa dola 9,200 pamoja na ambulance (gari la wagonjwa) mimi ndio niliyoita kwa kubaliana na Mbowe na Msigwa kwamba Turky haya mambo yasimamie baadaye…na ndicho kilichofanyika,” amesema.
Na Mwandishi Wetu
No comments:
Post a Comment