Mbunge Kubenea Aendelea Kusota na Polisi...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360..#share

MBUNGE wa Ubungo Saed Kubenea kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesafirishwa leo alfajiri kwenda mjini   akitokea  jijini Dar es Salaam, anaandika Mwandishi wetu.

Related image

Kubenea amefikishwa mjini Dodoma baada ya jana kukamatwa akiwa hospitali  jijini Dar es Salaam alipoenda kupata matibabu na kulazwa kituo cha Polisi cha Oysterbay kabla ya leo alfajiri kupandishwa ndege kwenda kutoa maelezo mbele ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge.

Mbunge huyo amekamatwa kwa amri ya Spika Job Ndugai ambaye wiki iliyopita aliviagiza vyombo vya dola kumsaka popote alipo Mbunge huyo na kumkamata.

Kosa la kukamatwa Kubenea lilitokana na kutofautina na Spika kuhusu idadi halisi ya risasi alizopigwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu mjini Dodoma .

Mbunge huyo alisema Lissu alipigwa risasi 38, huku Spika akisema idadi  ilikuwa 32 na baada ya kupishana huko, aliagiza Kubenea akamatwe ili akatoe ushahidi kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge ambayo pia inaendelea kuchunguza tukio hilo.

Kukamtwa kwa Kubenea kunaonekana kama Sinema ambayo imezoelekwa kwa kuwa siyo mara ya kwanza wabunge wa upinzani kusafirishwa kwa ndege chini ya ulinzi mkali wa polisi.

Miongoni waliowahi kusafirishwa kwa ndege ni pamoja na Ester Bulaya  ambaye ni Mbunge wa Bunda (Chadema),  kwa amri ya Spika pamoja na Freeman Mbowe aliyesafirishwa kwa ndege pia kwenda jijini Arusha kuhudhuria kwenye kesi.

Taarifa zinasema Kubenea amewasili leo mjini Dodoma saa moja asubuhi na kwamba badio afya yake siyo nzuri na hivyo hajui kama anaweza kusimama na kuhojiwa na kamati hiyo.

Aidha, taarifa hiyo imesema Kubenea bado ana maumivu makali sana na kwamba hajaambiwa atahojiwa wapi na saa ngapi.

Kubenea amemshukuru Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na  Mandeleo ya Makazi, Angelina Mabula ambaye amesema amesaidia katika hali yake ya ugonjwa mpaka kufika Dodoma baada ya kukutana naye kwenye ndege leo asubuhi.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search