Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe Atoa Ujumbe Mzito Baada ya Kumuona Lissu... Soma Hapa kwa Undani zaidi.. #share

Mwisho wa wiki hii iliyomalizika nilikuwa Nairobi kwaajili ya kumsabahi ndugu yetu Tundu Lissu, siku mbili hizi za kumuona Lissu kitandani pale zimeniacha nikifikiria sana. Nimerudi nchini nikiwa mwenye unyenyekevu zaidi kwasababu ya nguvu na ujasiri ambao ndugu yangu ameuonyesha licha ya kuwa kwenye maumivu makali.

Si mara nyingi hapa nchini utasikia tukiongelea ujasiri. Lakini namfikiria Lissu na vile nilivyojisikia nikiwa pamoja naye Nairobi. Najua hivyo ndivyo alivyo. Waliomshambulia wamemuumiza. Wamemuumiza kweli. Na bado wakati tuliokuwa naye amenionyesha shukrani, ari na pia ucheshi. Huo ni ujasiri.

Alichopitia na anachoendelea kupitia Lissu sio kitu rahisi kwa mtu yoyote kutafakari. Kufikiria hali ile kungeniacha nimeumia moyo Sana kama asingesema maneno haya kwangu "tumeshinda. Tumeshashinda".

Ujasiri ni Lissu

Kabwe Z. Ruyagwa Zitto
Kiongozi wa Chama - ACT Wazalendo
Septemba 18, 2017

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search