Mchungaji Mashimo Amtabiria Uhuru Kenyatta Kushinda Kiti cha Urais Kwa Mara Nyingine ....Habari Kamili Hii hapa na Matukio360....share..#


MCHUNGAJI wa Mitume na Maaskofu Tanzania David Mashimo (Komando Mashimo) amesema kuwa mgombea nafasi ya urais kupitia Mungano wa NASA Nchini Kenya Raila Odinga hawezi kuwa rais wa Taifa hilo kutokana maono aliyonyeshwa na Mungu.


Mchungaji huyo wa kanisa la True Gospel Seven day Church amesema hayo wakati wa mkutano wake na wanahabari uliuofanyika jijini Dar es salaam.

Amesema kuwa tangu novemba 26 mwaka Jana Mungu amemuonyesha maono kuwa Mgombea wa Urais kupitia chama cha Jubilee Uhuru kinyatta ataendelea kuwa rais wa Kenya licha ya mahakama ya Juu ya nchi hiyo kuzuia ushindi wa Kinyatta baada ya Odinga kushindwa kukubaliana na matokeo yaliyompa ushindi.

Komando mashimo  amesema kuwa Odinga hana mpango mzuri na nchi ya Kenya bali anatumiwa na makundi ya watu kwa maslahi binafsi.

Amesema kuwa jaji mkuu wa mahakama kuu ya Kenya Jaji Malaga ametoa hukumu hiyo kwa shinikizo la watu ambao hawaitakii mema nchi ya Kenya lakini akasisitiza kuwa Uhuru Kinyata atashinda kwa Mara      nyingine katika uchaguzi wa marudio kama ilivyotangazwa na tume ya uchaguzi ya nchi hiyo.

Pia amewaomba viongozi wa kiroho kuacha kuchanganya mambo ya dini na masuala ya kisiasa.

Komando mashimo amefanya tukio la kumpaka mafuta na kumwapisha Mwinjiristi na Mwimbaji wa Nyimbo za Dini Amon Mwakalukwa kama ishara ya kiimani ya ushindi wa Uhuru Kinyatta.

Na Abraham Ntambara


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search