Simba Yashindwa Kufurukuta Mbele ya Mbao Fc...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360..#share



Klabu ya Simba imeshindwa kufurukuta mbele ya Mbao Fc ya Jijini Mwanza baada ya kutoka sare ya 2-2.
Image may contain: one or more people, people playing sports, grass and outdoor

Katika mchezo huo uliochezwa uwanja wa CCM Kirumba Simba ndiyo ilikuwa wa kwanza kupata goli la kuongoza ambapo hadi kipindi cha kwanza kinaisha timu hiyo ilikuwa ikiongoza kwa goli hilo.
M
namo kipindi cha pili Mbao walianza kwa kasi na hatimaye kupata goli la kusawazisha lakini hazikupita hata dakika mbili Simba waliongeza goli lapili.

Wakati Mchezo ukiwa unaelekea mwishoni vijana dwa Mbao wameweza kuchomoa na mchezo kumalizika kwa sare hiyo.

Hiyo inakuwa ni sare ya pili kwa Simba kwa musimu huu wa ligi kuu ya VPL wakati kwa Mbao nsiyo kwa mara ya kwanza wanapata pointi.

Magoli ya Mbao FC yamewekwa kimiani na Kiyombo dakika ya 47 na Maganga dakika ya 81 huku yale ya Simba SC yakifungwa na Kichuya dakika ya 16 na Kotei dakika ya 49.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search