Mkutano wa ALAT Kufanyika Oktoba Mkoani Mbeya....Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360...#share

JUMUIYA ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT) imesema Mkutano Mkuu wa jumuiya hiyo unatarajiwa kufanyika mkoani Mbeya kuanzia Oktoba 2 hadi 5 huku ikibainisha Benki ya NMB imetoa Sh milioni 100 kwa ajili ya kufadhili mkutano huo.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar na Kaimu Katibu Mkuu wa ALAT, Abdallah Ngobi wakati akipokea fedha za ufadhili wa mikutano kutoka kwa benki hiyo.

Amesesema  mkutano huo utashirikisha wajumbe 500 kutoka mikoa mbalimbali huku akisisitiza miongoni mwa ajenda zitakazojadiliwa ni kuzishinikiza halmashauri zote kutenga fedha kwa ajili ya viwanda vidogo vidogo lengo likiwa kufikia uchumi wa kati wa viwanda.

“ Ajenda mbalimbali zitajadiliwa zikiwemo za kuzihimiza Halmashauri kuwa na utaratibu wa kuwa na maeneo yatayojengwa viwanda vidogo, ufafanuzi wa  utendaji kazi wa Wakala wa Barabara wa Mijini na Vijijini (Tarura),” alisema Ngobi.

Amebainisha kuwa katika mkutano huo Halmashauri zitaelekezwa jinsi ya kusimamia na kufanya kazi na Tarura hasa walengwa wakiwa wenyeviti wa serikali hizo , watendaji ina mameya.

Amefafanua kuwa jumuia hiyo inapongeza utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano kwa jinsi inavyoendesha nchi ikiwemo kusimamia ukusanyaji mapato, kupambana na ufisadi, rushwa na uwajibikaji.

Ameipongeza na kuishukuru  benki hiyo kwa msaada huo huku akiiomba iendelee kuisaidia ALAT katika kufanikisha mambo mbalimbali yenye manufaa kwa taifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Wateja Wakubwa wa benki hiyo, Richard Makungwa amesema NMB inatambua mchango wa ALAT na kwamba katika Halmashauri 185 imefunga mashine za kielektroniki 170.

Amesesma benki hiyo itaendelea kuifadhili ALAT  na kuweka wazi NMB ina kitengo maalumu cha kuwasaidia wafanyabiashara wadogo wadogo kwa kuwapatia mikopo ya kupanua Biashara zao.

Na Hussein Ndubikile


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search