Mwenyekiti Chadema Mbowe Aivaa Serikali Kuhusu Kumtibu Lissu...Habari Kamili na Matukio360...#share
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe amezungumza leo jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari kwa mara ya kwanza baada ya kurudi Dar es Salaam
kutoka Nairobi anakopatiwa matibabu Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu
aliyeshambuliwa kwa risasi September 7, 2017 jijini Dodoma na watu
wasiojulikana.
Mbowe ameeleza hali ya Lissu.
"Shambulio lile halikuwa kwa
Lissu peke yake, lilikuwa shambulio la Chama, kauli ya Haki, Ubinadamu na
Watanzania kupitia Lisu." Mbowe.
"Lissu amebeba majeraha
mengi, maumivu makali kwa kauli zake za kulitetea Taifa lake, kuwatetea
Watanzania wenzake na kudai haki." Mbowe.
"Nianze na habari njema;
Tundu Lissu anawasalimu sana. Nimeachana naye Nairobi jana mchana nikamwambia
nitazungumza na Watanzania." Mbowe.
"Akaniomba nimpelekee salamu
zake kwamba Mungu anaendelea kumpigania na In Shaa Allah baada ya muda atarejea
kwa mapenzi yake." Mbowe.
"Tundu Lissu yupo chini ya
ulinzi mkali sana saa 24 nje na ndani... hatuwezi kufanya uzembe tena" - Mbowe.
"Mashine yetu 'Lissu'
itarudi barabarani salama kabisa ikiwa timamu, nataka niwaeleze ufahamu wake
uko vizuri 100%"
"Lissu hakukata kauli mpaka
anaingia theatre, pamoja na majeraha yote hajawahi kukata kauli" - Mbowe.
"Hali ya mgonjwa, Lissu
alifikishwa Nairobi usiku saa sana, hali yake ilikuwa ngumu sana. Madaktari
walitupokea na kuanza kumhudumia." Mbowe
"Madaktari wanasema ni
miujiza kutoka salama bila kukatwakatwa kwa risasi ktk shambulio kama la
Lissu" Mbowe.
"Lissu anatibiwa na kundi
kubwa la madaktari na ningependa niwatambue waingie kwenye rekodi kwa kazi ya
ziada kuokoa maisha ya Lissu." Mbowe
"Kabla ya madaktari wa
Nairobi, niwashukuru madaktari wa Hospitali ya Dodoma. Kama wasingefanya wajibu
wao wa msingi tusingesafiri na Lissu"
"Kazi kubwa iliyofanywa na
madaktari wa dodoma tusiipuuze, ilituwezesha kufika Nairobi akiwa hai. Ilikuwa
ni miujiza kila mmoja alishangaa."
"Ikasemwa Ndege ya Lissu
imelipiwa na wanaCCM, hata ingelipiwa na CCM bado si shida ila ukweli imelipiwa
na Chadema" Mbowe.
"Kuna presha ya kumpeleka
nchi tofauti sita; wapo waliotaka apelekwe A. Kusini, wengine India, Ubelgiji,
Ujerumani, UK na USA" Mbowe
"Kama kiongozi wa Chama
nadiriki kusema kwamba mshukiwa namba moja wa shambulio la Lissu ni vyombo vya
ulinzi na usalama wa nchi hii" Mbowe.
"Hilo nalisema bila
kumung'unya maneno, viashiria vyote vya tukio lile tangu linatokea kauli na
kusita kwa viongozi na kauli za kujiosha."
"Ni nani katika vyombo vya
ulinzi na usalama, simjui lakini ni vigumu sana kusema tukio la ujambazi,
hakuna ujambazi pale." Mbowe.
"Watu wetu wamepotea, watu
wetu wameuawa, wanapigwa risasi mchana kweupe na hakuna hatua ya maana
inayofanyika." Mbowe.
"Michango ya TZ ni mil.52,
mil.43 zilizochangwa Bungeni bado hatujapewa, wa Marekani wamemchangia Lissu
USD 20000"
"Nimalizie kwa gharama za
matibabu. Hakuna kificho kila kitu kimewekwa humu. Mpaka juzi gharama zilifikia
Ksh Milioni 6.7." Mbowe.
"Ksh Milioni 7.4 ni sawa na
Tsh Milioni 162.8 kwa wiki mbili za matibabu lakini tunasema hata zingekuwa
Bilioni, zimemuokoa Lissu." Mbowe.
No comments:
Post a Comment