PM Awatumia Salamu Watu Wasiojulikana....Asema Serikali Haita....#share


WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema serikali haitafumbia macho matukio ya mashambulizi wanayofanyiwa watu mbalimbali wakiwepo viongozi na kuwataka wabunge na wananchi kuendelea kuwa wavumilivu wakati jeshi la polisi likiendelea kufanya uchunguzi.


Waziri Majaliwa amesema hayo wakati akiahirisha vikao vya mkutano wa nane wa bunge la 11, na kusema vyombo vya dola vinaendelea kufanya uchunguzi ili kuwabaini watu wasiojulikana wanaojihusisha na vitendo hivyo  ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

"Serikali haitofumbia macho matukio ya kihalifu yanayotokea nchini, vyombo vya dola tayari vimeshaagizwa kuhakikisha wanawatafuta wanaohusika na vitendo vya kihalifu na kukamatwa ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao", amesema Waziri Majaliwa.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama Adad Rajabu ameliomba bunge kuongeza muda ili kuweza kukamilisha kazi ya kufanya uchunguzi wa matukio ya kujeruhiwa, kuvamiwa pamoja na kufuatiliwa kwa baadhi ya wabunge ili kuweza kukamilisha kazi hiyo.

Aidha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amehairisha vikao vya bunge leo hadi  Septemba 7 mwaka huu ambapo litafunguliwa tena.

Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search