Rais wa Zamani TFF Malinzi, Wenzake Kuendelea Kusota Rumande...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360..#share

RAIS wa zamani wa Shirikisho la Soka Tanzanai (TFF) Jamal Malinzi na wenzake wanaendelea kusota rumande baada ya kesi yao kuahirishwa kutokana na upelelezi wa kesi yao kutokamilika.
Image result for jamali malinzi mahakamani
Malinzi na wenzake wanakabiliwa na mashitaka 28, ikiwemo ya utakatishaji fedha ambazo ni Dola za Marekani, 375,418.

Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU, Leornad Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, hivyo anaomba iahirishwe hadi tarehe nyingine.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Mwambapa ameahirisha kesi hiyo hadi October 5, 2017.

Mbali ya Malinzi, washitakiwa wengine ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mhasibu wa Shirikisho hilo, Nsiande Mwanga ambao wanakabiliwa na mashitaka 28, ikiwemo ya utakatishaji fedha ambazo ni Dola za Marekani, 375,418.


Na Mwandishi Wetu.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search