sPORTS nEWS: Je Simba kama Yanga Nayo kuvutwa Shati na Matajiri wa Madini Mwadui?... Ni leo baada ya dakika 90..#share

KLABU ya Simba SC ambayo inatajwa kuwa na kikosi cha gharama Zaidi leo inajitupa uwanjani katika mchezo wa raundi ya tatu katika mchezo wa Ligi Kuu Soka Vodacom Tanzania Bara kukabiliana na Matajiri wa Madini ya Almasi kutoka mkoani Shinyanga Mwadui FC.
Image result for simba vs mwadui
Mchezo huu utapigwa leo katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam majira ya saa 10.00 jioni. Itakumbukwa mechi ya kwanza Simba ilishinda goli 7-0 dhidi ya kikosi cha Ruvu Shooting na kasha kutoka suluhu baina yake na Azam FC.

Wakati matokeo ya Simba katika mechi mbili za awali yakiwa hivyo kwa upande wa Mwadui FC  kwenye mechi mbili za awali wameshinda moja na kupoteza moja.

Itakumbukwa jana klabu ya Yanga ilivutwa shati na klabu ya Maji maji ya Songea kwa kulazimishwa sale ya goli 1-1. Hivyo Simba itaingia ikihitaji kuwa furahisha mashabiki wake ili kuwazodoa mashabiki wa Yanga.

Je nani atakuwa ibuka mshindi katika mtanange huo. Je Okwi ataibebe Simba? Tusubiri tuone baada ya dakika 90.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search