Kumbilamoto awataka wakazi Ilala kujiandaa kwa mikopo...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

WAKAZI wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala jinini Dar es Salaam, wametakiwa kujiandaa kuchukua mikopo ya halmsahuri inayotarajiwa kuanza kutolewa hivi karibuni ili iwasaidie  kujikwamua kiuchumi.
Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akizungumza na baadhi ya wakazi wa Vingunguti jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa jana jijini humo na Naibu Meya wa Halmashauri ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Vingunguti Omary Kumbilamoto alipokuwa akizungumza na wakazi wa kata hiyo.

“Kwa hiyo sasa tupo kwenye michakato ya kujua je itumike benki hii ya DCB au tutoke tutumie CRDB au tutaangalia benki gani ambayo itakuwa na faida,” amesema Kumbilamoto.

Kumbilamoto amesema fedha hizo zilizotengwa kwa ajili ya wananchi ni takribani zaidi ya bilioni tano na itatolewa kwa akina mama asilimia 4, vijana asilimia 4 na asilimia 2 kwa walemavu.

Amesisitiza kuwa mikopo hiyo itatolewa kwa vikundi vya kuanzia watu watano ambapo amesema utaratibu utakapokamilika wakuanza kutolewa kwa mikopo hiyo watawatangazia.

Akizungumzia kuhusu miundombinu ya barabara amesema, barabara ya kwa Mnyamani ipokatika hatua za mwisho kuanza matengenezo kwani mkandarasi amekwishapatikana na ipo chini ya usimamizi wa Tarula.

Kwa upande mwingine Naibu Meya huyo ametoa misaada ya zaidi ya. Sh. milioni 2 kwa vikundi mbalimbali vya wajasiliamali na timu za mpira wa miguu.

Kwa upande wa wananchi wa kata hiyo, wamempongeza Diwani huyo kwa kuwa karibu nao kwa kuwapatia misaada hiyo na kuahidi kuendelea kushirikiana naye kwa ajili ya kujiletea maendeleo.

Matukio katika picha









About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search