sPORTS nEWS: Mwamuzi Simba na Yanga kuziamua Stars Botswana Uhuru kesho ........#share

MWAMUZI wa kimataifa, Elly Sasii atachezesha mchezo wa
kirafiki kati ya Taifa Stars ya Tanzania na Zebras ‘Pundamilia’ ya Botswana
kesho kwenye uwanja wa Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Elly Sasii ambaye alichezesha mchezo wa Ngao ya Jamii
hivi karibuni ambao Simba iliifunga kwa mikwaju ya penalti 5-4 atasaidiwa
na Soud Lillah (Line 1) na Frank Komba (Line 2) wakati mwamuzi wa akiba (Forth
Official) atakuwa Israel Nkongo.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF), mchezo huo utaanza saa 10.00 jioni, kiingilio ni
sh. 10,000 kwa Jukwaa Kuu na sh. 5,000 kwa mzunguko.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga leo Ijumaa
amezungumza na wanahabari kwenye Ukumbi wa Hosteli ya TFF, Karume jijini Dar es
Salaam ambako amethibitisha kwamba kikosi chake kiko imara kwa mapambano.
Kocha wa Botswana, David Bright amesema ingawa hana muda
mrefu kwenye timu ameteua kikosi chenye mchanganyiko wa vijana na wazoefu
aliokuja nao kuwajaribu .
Wachezaji wa Tanzania wanaocheza soka nje waliofika ni
nahodha Mbwana Samatta (KRC Genk/Ubelgiji), Elias Maguli (Dhofar FC/Oman), Abdi
Banda (Baroka FC/Afrika Kusini), Hamis Abdallah (Sony Sugar/Kenya),Farid Mussa
(CD Tenerif/Hispania) na Simon Msuva (Difaa El Jadidah ya Morocco).
Wengine ni makipa Aishi Manula (Simba), Mwadini Ally
(Azam FC) na Ramadhani Kabwili (Yanga).
Pia wamo Walinzi ni Gadiel Michael (Yanga), Boniphas Maganga (Mbao FC), Kelvin Yondani (Yanga), Salim Mbonde (Simba) na Erasto Nyoni (Simba).
Pia wamo Walinzi ni Gadiel Michael (Yanga), Boniphas Maganga (Mbao FC), Kelvin Yondani (Yanga), Salim Mbonde (Simba) na Erasto Nyoni (Simba).
Viungo ni Himid Mao - Nahodha Msaidizi (Azam FC), Mzamiru Yassin (Simba), Said Ndemla (Simba), Shiza Kichuya (Simba), wakati Washambuliaji ni Raphael Daud (Yanga), Kelvin Sabato (Azam FC) na Emmanuel Martin (Yanga).
Na Mwandishi Wetu
No comments:
Post a Comment