Sports News: Sakata la Neymar na Cavanni Lachukua Sura Mpya...Ni Baada ya Cavanni Kupuuza Ombi la Mabosi wake wa PSG..Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360..#share

KUFUATIA kutoelewana baina ya wachezaji wawili wa klabu ya PSG Edison Cavanni na Neymar kulikotokana na hali ya kutofautiana kwa kugombania kupiga peneti kulikotokea hivi karibuni.
Image result for neymar vs cavani
Ni kwamba taarifa hizo zinaendelea kutawala vichwa vya habari, baada ya mvurugano huo ambpo siku kadhaa zilizopita inasemekana wachezaji hao walipatana baada ya Neyma kuomba msamaha kwa kitendo hicho.

Hata hivyo kumeibuka jipya, inasemekana mabosi wa klabu ya PSG walikaa chini na Edison Cavanni na kumuomba amruhusu Neymar kupiga penati huku pia wakitaka kumpa kiasi cha pesa ili kukubali.

PSG walitaka kumpa Cavanni kiasi cha €1million ambayo ni pesa ambayo wangempa Cavanni mwisho wa msimu kama akimalizia mfungaji bora lakini sasa wakataka kumpa kiasi hicho ili amuachie Neymar kupiga tuta.

Edison Cavanni amekataa kiasi hicho cha pesa na hii inamaanisha kwamba hayuko tayari kumuachia mtu mwingine apige penati na anaona ni bora akose kiasi hicho cha pesa kuliko kuacha kupiga penati.

Inadaiwa kwamba baada ya Neymar na Cavanni kugombana ilimbidi tajiri wa PSG Nasser El Khaifi kukaa na Cavanni ili kujaribu kumshawishi kuhusu kumpa Neymar penati lakini Cavanni amekataa.

Mbaya zaidi inadaiwa kwa sasa kumeanza kuwa na makundi katika klabu hiyo kwani kuna kundi kubwa ndani ya PSG linalomsuport Cavanni huku kikundi kingine kidogo kinachoundwa na Wabrazil pekea yao wakiwa wanamuunga Neymar.

Hali hii inamuweka njia panda kocha wa klabu hiyo Unai Emery kwani ni wazi na yeye anataka Cavanni aendelee kupiga penati katika timu hiyo lakini tajiri wa timu anaonekana anataka Neymar awe kila kitu.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search