TCRA Yawataka Wanachi Kufahamu Matumizi ya Sahihi ya Mitandao...Habari Kamili Hii Hapa na Matukio360..#share


MAMLAMA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewataka Wananchi kuwa na ufahamu kuhusu matumizi sahihi ya mitandao ya kompyuta na Internent.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Meneja wa Mawasiliano TCRA Semu Mwakanjala akizungumza na waandishi wa habari, amesema ufahamu huo utawasaidia kukabiliana uhalifu wa kimtandao.

Amesema wanatoa ushauri wa kitaaluma wa kukabiliana na matukio ya kiusalama yanayotokea kwa lengo la kuzuia madhara.

“Tunawasihi watu wasijibu jumbe wanazopokea kwenye akaunti zao za barua pepe au ujumbe mfupi bila kuhakiki uhalali wa taarifa” amesema Mwakanjala.

Hata hivyo amesema mtu hatakiwi kufungua Link anayotumiwa na mtu asiyemjua bila kuhakiki ni kitu gani kilichotimwa.

Aidha amewatahadharisha watu waache kusambaza ujumbe wenye uzushi, uchochezi na chuki kwani hatua kali zitachukuliwa.

Amesema watu waache kutungeneneza akaunti za mitandao kwa lengo la kufanya utapeli na ulaghai na taarifa za uongo.


Na Mwandishi Wetu

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search