UPDATES: Marekani nayo yajitosa 'shooting' ya Tundu Lissu na kulaani vikali #share

NCHI ya Marekani imeeleza kusikitishwa kwake na tukio la kushambuliwa kwa risasi kwa Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) NA Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ubalozi wa nchi hiyo nchini kupitia ukurasa wake wa Facebook leo umelaani kitendo hicho cha kutumia nguvu.

“Tunalaani kitendo hiki cha kipuuzi na cha kutumia nguvu,” imesema taarifa hiyo.

Ubalozi huo umesema unaungana na Watanzania katika kumtakia kheri Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) ili apone haraka.

Lissu jana majira ya mchana akiwa ndani ya gari nyumbani kwake mkoani Dodoma alishambuliwa kwa kupigwa risasi na watu wasio julikana na kupatiwa matibabu ya awali katika holspitali ya rufaa ya Dodoma.

Aidha saa sita usiku alisafirishwa kwa matibabu zaidi katika Hospitali ya Aga Khan iliyopo Nairobi, Kenya.

Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema leo Ijumaa asubuhi kuwa, Lissu alishambuliwa kwa risasi kati ya 28 hadi 32, huku tano zikimpata mwilini.

Akitoa taarifa ya tukio hilo kwenye kikao cha Bunge, Ndugai amesema risasi mbili zilimpata Lissu kwenye miguu, mbili tumboni na moja kwenye mkono.


Na Mwandishi Wetu.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search