Waziri Mwijage Mgeni Rasmi Maadhimisho Tamasha la Wanawake Wajasiriamali..Habari Kamili na Matukio360..#share
Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika
Maadhimisho ya Tamasha la Wanawake Wajasiriamali(Mowe) litakalofanyika kuanzia
Oktoba 24 hadi 30 mwaka huu katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es
Salaam.
Hayo yamesemwa leo jijini humo na Mwenyekiti wa Mowe, Zubeda
Kiluwa wakati akitoa ufafanuzi kwa wanahabari juu ya taratibu na mpangilio
mzima wa tamasha utakavyokuwa.
Amesema Waziri Mwijage
ndiye atakayefungua maadhimisho hayo huku akisisitiza lengo kuu la tamasha hilo ni kuwahamasisha wanawake
kujishughulisha na shughuli za kiuchumi za kuwaingizia kipato kwa kutumia fursa
za kibiashara na rasilimali zilizopo.
“Wanawake wote popote walipo waje washiriki siku hiyo wataonyesha na kutangaza bidhaa na huduma
mbalimbali wanazozifanya kwa lengo la kupanua wigo wa masoko,” amesema Kiluwa.
Amesisitiza kuwa wanawake wajasiriamali watapata fursa ya
kujifunza na kukabiliana na ujuzi na uzoefu wa stadi mbalimbali na kwamba
tamasha hilo limebeba kauli mbiu inayosema ‘Mwanamke Mjasiriamali funguka shiriki kujenga
Tanzania ya Viwanda’.
Aidha, amesema washiriki wa tamasha hilo watatakiwa kulipa
gharama ya ushiriki sh 50,000 na kuwataka wananchi wajitokeze kwa wingi katika
viwanja hivyo ili waweze kujionea bidhaa zinazozalishwa na wanawake hao.
Amebainisha kuwa tamasha hilo halitahusisha wanawake
wajasiriamali kutoka nchini pekee bali wengine watatoka nchi jirani za Kenya,
Uganda, Burundi, na Rwanda pamoja na mataifa mengine ya Afrika.
Na Hussein Ndubikile
No comments:
Post a Comment