ACT Wazalendo kuwasilisha hoja Bungeni dhidi ya Serikali ..soma habari kamili na Matukio360...#share
Na Mwandishi wetu
CHAMA cha ACT Wazalendo kinatarajia kuwasilisha hoja Bungeni ikishutumu Serikali kuchukua fedha kinyemela kwenye Mashirika ya Umma kinyume na utaratibu na sharia.
Mhe Zitto Kabwe
Taarifa iliyotolewa na kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe imeandika “ ACT Wazalendo kinatarajia kuwasilisha Hoja Bungeni kwa Serikali kuchota Fedha za Mashirika ya Umma kinyume cha Sheria.”
Taarifa hiyo hajatoa maelezo kwa kina na bila kutaja majina ya mashirika hayo lakini kimsingi mwasilishaji hoja hiyo ni Zitto mwenyewe kwa kuwa ndie mbunge pekee wa chama hicho Bungeni.
Zitto aliwahi kuwa mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya mahesabu ya mashirika ya umma kwa kipindi cha miaka 10.
Uenda hoja hiyo ikiwasilishwa mwaka huu au mwakani kulingana na utaratibu wa Bunge unavyoelekeza.
CHAMA cha ACT Wazalendo kinatarajia kuwasilisha hoja Bungeni ikishutumu Serikali kuchukua fedha kinyemela kwenye Mashirika ya Umma kinyume na utaratibu na sharia.
Mhe Zitto Kabwe
Taarifa iliyotolewa na kiongozi wa chama hicho, Zitto Kabwe imeandika “ ACT Wazalendo kinatarajia kuwasilisha Hoja Bungeni kwa Serikali kuchota Fedha za Mashirika ya Umma kinyume cha Sheria.”
Taarifa hiyo hajatoa maelezo kwa kina na bila kutaja majina ya mashirika hayo lakini kimsingi mwasilishaji hoja hiyo ni Zitto mwenyewe kwa kuwa ndie mbunge pekee wa chama hicho Bungeni.
Zitto aliwahi kuwa mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya mahesabu ya mashirika ya umma kwa kipindi cha miaka 10.
Uenda hoja hiyo ikiwasilishwa mwaka huu au mwakani kulingana na utaratibu wa Bunge unavyoelekeza.
No comments:
Post a Comment